15 February 2011

Bora nipigwe risasi kuliko kufuta kauli-Lema

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

MBUNGE wa Arusha mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Mendeleo (CHADEMA), Bw. Godbles Lema amesema kuwa yupo radhi achague
kupigwa risasi kuliko kufuta kauli yake aliyotoa bungeni wiki iliyopita kuwa Waziri Mkuu amesema uongo kwa kuwa ana ushahidi kwa asilimia mia moja na ana uhakika nao.

Kauli ya mbunge huyo ambayo ilisababisha Spika Anne Makinda kumtaka athibitishe kauli hiyo kwa maandishi kufikia jana, aliitoa Februari 10, mwaka huu bungeni akidai kuwa Waziri Mkuu amelidanganya bunge kuhusiana na mauaji ya Arusha.

Akizungumza na gazeti hili jana, Bw. Lema alibainisha kuwa alikuwa tayari kusoma uthibitisho wake bungeni jana lakini cha kushangaza ni kwamba spika amemtaka awasilishe katika ofisi yake kwa maandishi.

“Mimi nilikuwa tayari na ushahidi wangu na bado nipo vizuri, nilikuwa niwasilishe ushahidi wangu bungeni, sasa naambiwa niwasilishe ushahidi wangu ofisini kwa spika, nipo radhi nichague kupigwa risasi kuliko kufuta kauli yangu ambayo niliitoa hivi karibuni bungeni, kwa kuwa nina ushahidi wa
uhakika,” alisema Bw. Lema.

Hata hivyo, baada ya kuzungumza na waandishi wa habari, mbunge huyo alikataa kuulizwa maswali kuhusu kilichomo kwenye ushahidi wake.

28 comments:

  1. wabunge chadema simamieni maslahi ya wanyonge tuko nyuma yenu

    ReplyDelete
  2. ni kukomaa ccm ishaoza hata huyo pinda ameoza

    ReplyDelete
  3. Madikteta wote wana tabia moja; huwa hawana uwezo wa kugundua kuwa wamepoteza mamlaka ya kutawala. chama tawala hakina wafuasi tena na wabunge wa chama tawala wameng'ang'ania kanuni na taratibu za bunge lakini Mamlaka imeshawatoka!

    ReplyDelete
  4. eng.mwakapango, E.P.AFebruary 15, 2011 at 9:22 AM

    jana nilimsikia mbunge Bura wa viti maalum CCM akisema damu ya watanznia iliyomwagika na iwe juu yenu. Kauli hii niliipenda sana kwa sababu inaonyesha ni jinsi gani mwanadada huyu anavyojua kutumia philosofia ya kulaani watawala. infact alikuwa anawalaani CCM ambao walitumia nguvu kuzima maandamano ya CHADEMA huku wakijua kuandamana ni haki ya msingi na ya kikatiba na hivyo CHADEMA ilikuwa sahihi. na ukitazama kwa makini hapa CCM ndiyo wanaotafuta madaraka kwa sifa, kuonyesha kiburi cha dola kwa kuvijaribu vifaa walivvyopewa msaada na mabeberu wenye nia ya kumaliza madini yetu yote ni. mbona hatukuona maji ya kuwasha, mobomu ya machozi na risasi za moto misri na Tunisia ambako hali ilikuwa tete kuliko Arusha? mauaji ya wananchi yalifanywa kwa watu ambao hakuwapo kwenye maandamo tuaambiwa mmoja alikuwa anatoka kununua spare parts. Mizengo Pinda anaelkea kuichafua CV yake ambayo watanzania bila kujali itikadi zetu tunaikubali amejiingiza kwenye siasa za vyama wakati yeye ni mtendaji mkuu wa serikali nani hakuona kwenye vyombo vya habari jinsi unproffesional policemen walivyokuwa wakipiga ovyo magari utadhani wamevutishwa bangi. Mizengo Pinda alitakiwa atumie nafasi hiyo bungeni kukemea utendaji mbovu wa jeshi la polisi na siyo vibaya kama angewaomba radhi CHADEMA kwa upungufu huo. hivi leo Godbless Lema akithibitisha waziri mkuu mwongo si itakuwa aibu kubwa kwa serikali?. mimi nmwomba Anne Makinda aachane na hilo jambo kidiplomasia ili kutomshushia hadhi waziri mkuu wetu mpendwa.

    ReplyDelete
  5. mikanda ya video vya kilichojiri arusha ipo tele,naomba lema atoe ikibidi waziri mkuu kujiuzulu aachie ngazi ni mwongo na hatuwezi kuwa na waziri mkuu mwongo.huo ukweli upo,wakazi wa arusha tunaujua sana hata kuliko pinda kwani sisi ni waathirika wakuu.ili sio jambo la kusema thibitisha au laa.sisi tulio mashaidi tunasimama kumtetea lema na akitaka udhibitisho mwingine ambao hana tutampatia.hongera mbunge wetu.

    ReplyDelete
  6. HONGERA LEMA TUNAJUA ULISEMA UKWELI NA WAZIRI MKUU ALIDANGANYA BUNGE, KWANI YALIYOFANYIKA KILA MTU ALIONA NA SHERIA ZILIZOKIUKWA KILA MTU ANAJUA NA WASIFIKIRI WATANZANIA WA SASA NI WAVIVU KUSOMA SHERIA? CCM NA POLICE DAMU YA WATU ILIYOMWAGWA KWA UROHO NA DHAMBI ZENU UWARUDIE NA KUWAHANGAISHA MILELE. PINDA UMEJIPOTEZEA HADHI KUBARIKI UJINGA WA ARUSHA KUJIFANYA UNAJUA KILA KITU ETI SERIKALI IKO MAKINI JE KUANDAMANA BILA RISASI NA KUANDAMANA NA KUPIGA RISASI NI KIPI BORA NA NI KIPI KILIWATIA HOFU WATALII?? NA NI WAPI USUMBUFU ULIJITOKEZA?? KUUA RAIA NA MAZISHI YALIYOFANYIKA YA HESHIMA MBONA MAANDAMANO YALIKUWA YA AMANI..............ACHENI KUHADAA WATANZANIA NA ACHENI KUFURAHIA VIFO VYA WATANZANIA WENZETU,SASA ANGALIA MMEABIKA BAADA YA KUONA UKWELI KUWA ULIDANGANYA NA KUMZUIA LEMA KUTOA USHAHIDI.

    ReplyDelete
  7. Madam Spika ameshagwaya. Alifikiri Lema ni wa kada ya analogue, na kusahau kuwa Lema na kizazi cha digital ambacho kinafanya kazi kisayanzi zaidi. Kwa nini Anne Makinda anataka Lema apeleke maandishi ofisi ya Spika wakati alimtaka atoe ushahidi huo bungeni? CHADEMA wangetafuta forum wakaonesha mkanda wa vidoe wa yaliyojiri kwa wananchi ili uwongo ujitenge na ukweli. Wabunge wa CHADEMA endeleeni sana kuwakimbiza watawala wasaliti

    ReplyDelete
  8. nilimsikia madam spika akisema bunge haliendeshwi kwa magazeti bali kanuni.kanuni zipi sasa mbona anapindisha yeye?
    Kasema lema aleta ushahidi bungeni kwa maandishi,sasa anakwepa anasema apeleke ofisini,kwa nini isisomwe kama ya richmond.waliompa kiti wamezunguka wakaona ikisomwa italeta aibu kwa ccem.ifichwe sasa itawekwe kwenye mitandao tutaisoma tutaitolea mawazo yetu,yeye madam aiweke kwenye hazard zake ili lema aweze kuwa juu kama obama,hapo maza umechemka,itasomwa hadi dunia itaelewa yote,sasa umefanya nini,mami pole kwa hayo,na hongera lema kwa ujasiri.

    ReplyDelete
  9. ukweli huwa haufichwi madam ipo cku utawekwa hadharani kila mtu atwujua, ndio mtakapoumbuka ww na wana ccm wenzako.

    ReplyDelete
  10. huyo msenge anayesema pinda ameoza kaoza mama yake mjinga sana huyo na lema wake tena we ukome kwa maoni ya kijinga

    ReplyDelete
  11. KINEMBE KAMESHALEGEA, MNATEGEMEA NINI? HAKUNA MAAMUZI MWEMA YA HUYO. WEKA MWANAMUME HAPO.

    ReplyDelete
  12. Wewe mbwa unae kataa kwamba Pinda hajaoza inaonekana na wewe umeoza mbwa koko weeh

    ReplyDelete
  13. achane matusi jamani embu muwe wasomi na wachanganuaji wa maswala yenye maslahi ya nci na kuwa shabiki wa chama fulani ndugu zangu watanzania wenye kuzungumza lugha moja na maridhawa ya kiswahil, mizengo kayanza pita pinda amekosea tukubali amekosea na lema yuko sahihi bunge linako elekea ni kubaya kiukweli tunaitaji msaada wa kweli

    ReplyDelete
  14. NILISEMA CCM WAMESHAPOTEZA MAMLAKA YA KUTAWALA> HAKUNA MTAWALA HALALI ANAWEZA KUTUMIA MATUSI MAKUBWA KAMA HUYO ANONYMOUS WA FEB 15,2011 11:45 AM HUYO ALIYEANZA KUTUKANA WENZAKE NI CCM NA INAWEZEKANA NI USALAMA WA TAIFA AU POLISI. MTU KAMA HUYU HANA NEEMA YA MUNGU WALA MUNGU HAYUKO NA MTU KAMA HUYU. MTU HUYU ANAWAKILISHA UTAWALA ULIOKWISHA ANGUKA NA UMEKATALIWA NA MUNGU NA WANADAMU

    ReplyDelete
  15. Hili ni jalala la wahuni, Bunge ni pahala penye kanuni na taratibu. kama umeambiwa wasilisha kwa maandishi basi wasilisha hiyo kutamka hufuti kauli yako bora upigwe risasi inaletwa na nini,maana kauli ya kufuta kauli itategemea ushahidi utakaoutoa sasa wewe umegeuka mshtakiwa na hakimu hapohapo? Hapo utabadilika tu maana si vijiweni. Wee ni pumba tu hamna kitu hapo. Sogeleeni polisi kuvamia muone tena cha moto,huyo baba yenu Padri aliyewatuma muende polisi mkawatoe viongozi wenu ndio wa kubeba lawama zote na ushahidi wa kuwaambia mkafanye hivyo upo.

    ReplyDelete
  16. Ndio faida ya kuweka watu wa vijiweni kwenye nafasi kama ya Mbunge matokeo yake anafikiri mambo yanakwenda kivijiweni. Ushahidi hawana kwanza mpaka leo hawajapeleka ushahidi kibao kuhusu madai mbali mbali waliyotoa, mojawapo walisema wanaushahidi kura za urais zilichakachuliwa mpaka leo hii mwezi February hatuoni huo ushahidi hata kuchapishwa basi kwenye magazeti yao kama hili la majira.

    Peleka ushahidi ulioulizwa na si kupiga zumari barabarani. Na ukiwekwa pembeni ukakatwa posho ya siku 5, na uchaga wako na pesa mbele mwenyewe siku nyingine utafuata taratibu za bunge. Kazi kuleta uhuni uhuni tu wa mtaani bungeni. Hivi zile milioni 200 walizopewa na Saboko wafanye semina ya kuwaelimisha wabunge wa chadema na kuwanoa kwa masuala ya uongozi ndio zimeishia kwa kale kasemina ka Bagamoyo walikopigana ngumi mpaka wakataka kutoana meno?

    ReplyDelete
  17. Pale mlipokuwa mnasema nyie haja yenu ni ofisi za CCm na kituo cha polisi central kuvichoma moto mlikuwa mmekunywa mbege? nyie ni mafala tu mmeambiwa mkafanya bila kufikiri sasa yamewakuta mnaruka hamkuwa mmekusudia hivyo,ole wenu jaribuni tena muone. Paka shumi nyie

    ReplyDelete
  18. CHADEM we r behind you plz dont let us down. simamieni ukweli kufichua waliooza.

    ReplyDelete
  19. anonymous anayetetea upumbavu shule ndogo kabisa shule ndogo we call them dumb dumb mjinga kabisa unaleta siasa za pilau we ngoja dawa ipo watch it. Mungu ndiye anayeendesha Tanzania sio ccm na unatetea ujinga kwasababu hali yako kwanza ni dhofuu i have no doubt about that together we can go Chadema

    ReplyDelete
  20. wabongo sisi tulio nje ya nchi yetutumechoka kuona maoni yaliyojaa malumbano ,matusi ,kubezana na kubeza viongozi sasa tulifikiri tutasoma maoni ya jinsi gani viongozi wetu wafanye ili kuokoa taifa letu lisiangamie ,sasa nyie wenyewe mnatukanana bila sababu za msingi pia mmeng'ang'ania mambo ya vyama,kila mmoja anasifia chama na viongozi wake.jamani pendaneni mnaacha mpaka tunaogopa hata kusoma magazeti ili tujue nchi yetu inakwendaje!pia acheni kuifananisha tz na nchi kama tunisia na misri,sisi bado hatujafikia huko,tukae meza moja tujadili mambo mazuri ya nchi yetu.

    ReplyDelete
  21. wewe pia mjinga na huna akili na kama umesoma basi ni udsm chuo hakipo hata kwenye vyo bora 1000 duniani ndio ww mwenye akili ni yule alio waamrisha wajinga waende kuwakomboa wenzenu waliokamatwa nasi tuna sema tanzania sio chadema ccm wala chama chochote tanzania ni ya watanzania huna adabu kabisa

    ReplyDelete
  22. walikwenda kuvamaia kituo kwa akili za kuambiwa na padri slaa ambaye nae pia aliambiwa na mapadri wanasiasa wenzake pasipo kuchanganya na akili zao. waliopigwa risasi walistahili kufa kwa kutochanganya akili zao na walizoambiwa. pinda kaongea ukweli kuhusu meya wa Arusha kwani ccm ina madiwani 16 na CHAGADEMA 14 hata uchaguzi urudiwe kila siku ccm itashindwa. lakini kuna wajinga wa CHAGADEMA wanasema eti ni lazima madiwani wa CCM waipigie kura wenzao wa CCM je kuna diwani yeyote wa CHAGADEMA aliyepiga kura CCM hata kama hao wa CHAGADEMA wako wawili hawapigi kura CCM. CHAGADEMA acheni ujinga nchi hii haitawaliwa kwa nguvu ya kanisa kama mlivyobadilisaha usemi na kuita nguvu ya umma

    ReplyDelete
  23. CCM ni chama kilichopoteza dira mimi ninavyoona kwani imefikia hadi waziri mkuu anaongea pumba bungeni wakati anajua kabisa sheria zimekiukwa arusha kwenye uchaguzi wa meya.

    OK achilia mbali hata kama ccm itashinda why isiitishe uchaguzi upya ambao utakidhi sheria?

    Why mjumbe feki aingizwe kupiga kura? je madiwani walitimia 2/3 wanaotakiwa kutimia kuchagua meya? CCM ACHENI UBABAISHAJI KWANI MNAENDESHA NCHI KIHUNI ILA JIFUNZENI KWA WENZENU WA MISIRI NA SASA TANZANIA KUMEKUCHA

    Huyu mchangiaji wa hapo juu anatema pumba tupu kwani kama kauli ya spika ilikuwa sahihi why aogope hoja ya LEMA isisomwe bungeni ili wanchi tujue nani mwongo.

    Pinda amejipotezea hadhi sana!!!!!!!!!!!maana ndie alikuwa tumaini la ccm lakini leo amekuwa kichekesho bungeni kwa kudanganya umma eti serikali ipo makini wakati serikali imelala fofo imeachia madini yetu,samaki na misitu inaporwa na wageni kwa manufaa ya nchi zao. Pia DOWANS,RICHMOND,EPA,NBC na Mengine mengi yameingia wanakoroma na badala yake ccm na police wamebaki kuua raia bila hatia kila kukicha

    ReplyDelete
  24. Nyinyi polisi na CCM msifikiri sisi watanzania ya kuwa tunadanyanywa kama mabwege sisi sio mabwege. Matusi hayasaidii kwanza mnajidhalilisha na kuonyesha jinsi mlivyokabwa na uongo wenu. Hamtamwonea mtanzania kwa kutafuta haki. Ndio, nyinyi polisi na ccm mnawezaga kwa sababu mmedhiriki hata kutangazia umma mambo ya uwongo.

    ReplyDelete
  25. CCM ni Chama Cha Matusi. Kila anayeongea kutoka CCM anatukana matusi ya Nguoni. Mungu amewakataa na wananchi wamewakataa. Mamlaka imeshawatoka wamebakia na laana tu.

    ReplyDelete
  26. Weweeee, eti Mungu amewakataa CCM na nyie mnaokimbia masinagogi yenu na kukimbilia siasa mumemkataa Mungu au?

    Ujinga mtupu haya ya Mungu kwenye siasa yanaingiaje? Mlijidanganya mkatuma masala kibao eeh sijui haya huyo Mungu wenu kwanini aliwatupa wakati wa uchaguzi na hakumpa nchi padri muasi aongoze? Unajua kwanini Mungu alimnyima padri muasi kuongoza nchi hii? Mungu anajua kuwa kama padri muasi aliweza kumuasi Mungu na kuvunja ahadi yake aliyoiweka na Mungu atashindwaje kuvunja ahadi alizoweka na viumbe dhaifu kama binadamu.

    Kwa hiyo Mungu anatupenda na ndio maana ametulinda! Atupendaa atupendaa kweeli!!!

    Mnalo hilo! Uchaguzi umekwisha na huko Arusha Madiwani wa CCM ni zaidi ya wa Chadema nendeni mkajipange upya kwa ajili ya kugaragazwa tena mwaka 2015. Sisi wenzenu sasa hivi tunajiandaa na chaguzi za serikali za mitaa, nyie mmekalia kulumbana na kugombana wenyewe kwa wenyewe, hamna adabu wala heshima kwa wakubwa, hujasikia hata siku moja kijana wa ccm kampiga mtu mzima kwenye mkutano! Na nina uhakika wengi watawakimbia kwa upuuzi wenu na laana mnayo nyie msie jua kumuheshimu wala kumuogopa Mungu na mamlaka yake ndio mtaheshimu mamlaka za duniani?

    ReplyDelete
  27. nyie ccm acheni mambo ya kipuuzi kwani mnaowafanyia ubabe na kuwaongopea ndio wale waliowaamini na kuwakabidhi madaraka ,ambayo mnalingia na kuwatishia hao waliwakabidhi.Na nyinyi Polisi mliokosa Elimu ya kutosha na kupungukiwa uwezo wa kufikiri msiwe wajinga kupindukia.Polisi ni masikini wa elimu kwani wengi wao ni Form four failed na standard seven ya mkoloni,MJIFUNZE SHERIA NA MUACHE UBABE WA KUUA WATANZANIA WASIO NA HATIA ."PEOPLEs POWER!!!!!!

    ReplyDelete
  28. Watanzania umefika wakati wa kufanya mabadiliko ya kweli kwasababu ishara zote zinaonyesha ya kuwa CCM imeshindwa kuplay a crucial task as driver of this country,na sababu wanaongoza nchi kama familia kwani wakubwa hao waliojaa matumbo kwa sababu ya uroho wa madaraka na kuflat nyuma kwa safari za kila siku ,wameshindwa kabisa kuwa na ubinadaMU ,TO THE EXTENT THAT THEY KILL TANZANIANS WHO ARE INNOCENT,napenda kunukuu mahojiano ya Baba yetu mpendwa JK nyerere "CCM sikuzaliwa nayo wala si baba wala mama yangu na hivyo niko tayari kujitoa ikiwa wanasisiem watamuweka kiongozi mla RUSHWA" Mwalimu na sokoine walikuwa wazalendo na wachapa kazi ,hivi kwanini msichukue mfano huo !!!!!!!!

    ReplyDelete