David John na Penina Malundo
WAZIRI Mkuu wa Serikali wa Thailand, Yingluck Shinawatra,
anatarajia kuwasili nchini leo kwa ziara ya kikazi ambapo atapokelewa na
mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete, katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Mwalimu Julius Nyerere.
Akizungumza Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari
jana, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadik, alisema Waziri huyo
ambaye atawasili jijini saa 6.30 mchana atapokelewa na kukagua gwaride maalumu
na baadaye atasaini mikataba mbalimbali kati ya Serikali yake na Tanzania.
Sadik alisema ujio wa waziri huyo utasababisha baadhi ya barabara
kufungwa na kuwataka wananchi kuwa wavumilivu na kujitokeza kwa wingi kumpokea
kiongozi huyo.
" Tu n awa omb a r a d h i wananchi kwa usumbufu
utakaojitokeza kwani baadhi ya barabara zitatakiwa kufungwa kwa muda ili
kupisha msafara wa kiongozi huyo na barabara hizo Nyerere, Railway
Gerezani,Sokoine Drive hadi Ikulu."alisema
Aliongeza kuwa barabara hizo zitafungwa kuazia muda wa saa 6.00
mchana hadi 7.30 na katika kipindi hicho chote wananchi wanatakiwa kuwa
wastamilivu na kufuata maelekezo watakayokuwa wanapewa na Polisi hasa kwa
madereva.
Sadik aliongeza kuwa katika
kipindi chote atakachokuwa hapa nchini atapata fursa ya kutembelea mbuga ya
wanyama ya Serengeti kwa siku moja na baadaye atarejea mjini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment