02 July 2013

WAUMINI WATAKIWA KUONDOA UHASAMA MIONGONI WAO


 Na Daud Magesa, Mwanza

MWENYEKITI wa Msikiti wa Khoja Ithina Asheri, Mkoa wa Mwanza, Sibtain Meghjee amewataka waumini wa madhehebu mbalimbali ya Dini nchini, kujenga utamaduni wa kusoma, kujifunza mambo mazuri na kutunza aya za vitabu vya imani ya dini zao ili kuondoa uhasama na tofauti za kidini katika kujenga taifa lenye mshikamano.
Alisema waumini wa dini zote wanapaswa kujifunza vitabu vyao na vya dini nyingine na kuchukua mazuri yaliyomo kwa ajili ya jamii sababu hakuna sehemu yoyote katika vitabu hivyo iliyokashifu dini nyingine.
Meghjee alitoa rai hiyo mwishoni mwa wiki wakati wa kongamano la kuhifadhi Quran lililofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Mbugani jijini Mwanza.

Alisema Watanzania kutokana na imani tofauti ni vema wakajenga utamaduni wa kusoma vitabu vya dini zao na kuhifadhi ujumbe mzuri uliomo kwa manufaa ya jamii.
Meghjee alieleza kuwa waumini wakisoma vitabu vya dini zao na kusambaza ujumbe mzuri kwa jamii hakuna mahali Watanzania watahasimiana kwa misingi ya kukashifu dini nyingine.
"Kongamano hili limeandaliwa kutoa ujumbe mzuri kwa jamii ili kuondoa uhasama ulioibuka nchini kati ya waumini wa dini na dini kutokana na baadhi kutoa matusi yanayokashifu dini zingine," alisema.
Alisema taifa limekumbwa na mambo yanayotishia amani na ustawi wa wananchi wake ambao wameishi miaka mingi kama ndugu,lakini upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya watu kushindwa kusoma na kuhifadhi ujumbe mzuri wa vitabu vya dini unasababisha kuwepo kwa uhasama kati ya waumini wa dini moja na nyingine.

Meghjee alieleza katika kongamano hilo, walialika waumini wa dini mbalimbali kuja kushuhudia na kujifunza jinsi gani muumini anaweza kuhifadhi ujumbe uliomo katika vitabu vya dini yake kisha akausambaza kwa jamii iweze kujifunza.
"Tumefanya hivi maeneo mengi ya nchi yetu na mwitikio umekuwa mzuri, nia na lengo letu ni kuhamasisha waumini wa dini nyingine wasome vitabu vyao ikiwezekana na vya dini zingine ili wachukue mazuri na kuyasambaza kwa jamii.Tukifanya hivi tutaondokana na uhasama na mambo yanayotishia amani, ustawi wa dini zetu na taifa," alisema.
Katika kongamamno hilo, Mohamed Takihan (16) mwanafunzi wa masuala ya dini nchini Iran,alionesha umahiri wa kutunza aya mbalimbali za Quran Tukufu ambapo alijibu maswali aliyoulizwa kupitia kitabu hicho.
Takiihan ambaye ni yatima, alianza kuhifadhi aya mbalimbali za Quran akiwa na umri wa miaka 10 na bado angali anafanya hivyo amefanya hivyo mara hamsini

No comments:

Post a Comment