02 July 2013

WANANCHI WAHIMIZWA KILIMO CHA BIASHARA


WA N A N C H I Wi l a y a n i Mbulu,hususan wa kata ya Bashay Mkoani Manyara wamehimizwa kulima kilimo cha biashara zaidi ili kubadilisha mazingira waliyonayo, anaripoti Mary Margwe, Mbulu.

Hayo yalibainishwa jana na Mkuu wa Wilaya hiyo Bw.Anatory Choya wakati alipokuWa akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha wadau wakati akizindua programu ya miundombinu ya masoko na uongezaji wa thamani ya mazao na kuboresha asasi ndogo za kifedha Vijijini.
Alisema kuwa ni vizuri wananchi wanaotegemea zaidi kilimo cha zao la vitunguu swaumu kujipatia kipato wakalima kilimo cha kibiashara zaidi ili kuweza kubadiLisha mazingira waliyonayo sasa.
Bw.Choya alisema wananchi wa kata ya Bashay wamekua na mafanikio ya kupata kipato kikubwa kutokana ulimaji wa zao la vitunguu ambapo vinauzwa zaidi ndani na nje ya nchi ambalo linawasaidia kuendesha maisha yao.
Aidha, alifafanua kuwa licha ya kipato wanachopata wakulima hao lakini wamekua wakijiingiza kwenye migogoro isiyo ya lazima mara wavunapo zao hilo na kupata fedha,ikiwa ni pamoja na kuuza ng’ombe.


Aidha, kufuatia mradi huo unaopelekwa wilayani hapo Mkuu huyo aliwataka wananchi kuhakikisha wanathamini miradi mbalimbali inayopelekwa na Serikali pamoja na asasi mbalimbali kuhakikisha wanaitunza ili iweze kuwa endelevu na hatimaye kuweza kuwaletea mafanikio
Naye Afisa Kiungo wa Mradi wa Uongezaji wa thamani ya mazao na kuboresha Asasi Ndodondogo za Kifedha Vijijini (MIVARF) wa wilaya hiyo Bw. Gilba Constantino ,alisema Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Kitaifa la kusaidia Maendeleo Kilimo (IFAD) na Benki ya Maendeleo Afrika (AFDB), wanatekeleza programu ya miundombinu ya masoko ,ongezeko la thamani , na huduma za kifedha Vijijini(MIVARF).
Bw. Constantino alisema mpango huo ni wa miaka saba,ambo ulianza 2011-2017,mpango uliotokana na mradi uliotangulia ‘Agricultural Marketing Systems Development Programme (AMSDP) and Rural Finance’,na kusema kuwa lengo la mradi huo kupunguza umaskini kuongeza kasi ya maendeleo kiuchumi endelevu ikienda sambamba na malengo ya Kitaifa ya maendeleo kama Mkukuta/ Mkuza ,ASDP,ATI KILIMOKWANZA NA SAGGIT.

Aidha, alifafanua kuwa mradi huo una nia ya kuziwezesha kaya za wazalishaji kuongeza kipato na kuwa na uhakika wa chakula,ikiwa ni sambamba na kuwaunganisha wazalishaji hao na masoko,kuongeza thamani ya mazao na masoko ya mitaji kupitia asasi ndogo za kifedha Vijijini.
"Katika mradi huu wanufaika ama walengwa ni wazalishaji wadogo wasindikaji ,vikundi vya masoko,asasi ndogo za kifedha kama vile saccos,vikundi vya kuwekeza na kukopeshana, vicobasilc, ambapo alifafanua kuwa wanufaika wanategemewa kuongeza kipato na kuinua uchumi kwa ujumla,kuongeza ubora katika uzalishaji ili kupata bei nzuri ya mazao,kuwa na uhakika wa chakula,kuongeza uzalishaji wa mazao, kupunguza gharama za uzalishaji.

No comments:

Post a Comment