02 July 2013

TRA YAWAKUMBUSHA WALIPA KODI WAJIBU WAO


 Na Kassim Mahege

WATANZANIA wameshauriwa kulipa kodi kwa wakati ili kuharakisha maendeleo ya taifa pamoja na kuepusha usumbufu wa foleni dhidi yao.
Akizungumza na gazeti hili jana kwenye maonyesho ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba jijini Dar es Salaam, Ofisa Mwandamizi kwa Elimu ya Walipakodi Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Msafiri Mbibo alisema hiyo ni mojawapo ya changamoto wanazokumbana nazo.

"Kuna malalamiko mengi ikiwemo suala la msongamano wa watu wengi wanaposubiri kipindi cha mwisho cha kulipa kodi, ambapo kunakuwa na msongamano wa watu wengi na kusababisha usumbufu kwao," alisema.
Alisema, ni vyema kutosubiri kipindi cha mwisho kulipa kodi kwani wakati huo watu wengi huwa wanalipia, hivyo kusababisha kero.
Akifafanua zaidi alisema, TRA kazi zake kubwa ni kukadiria kiasi cha kulipakodi, kukusanya kodi ikiwemo kuwasilisha makusanyo ya walipa kodi kwa Serikali.

No comments:

Post a Comment