Na Mwandishi Wetu
WASOMI na wanasiasa nchini wameishukia
Serikali kuwa ndiyo inayochangia hali ya kuhatarisha amani ya nchi na kwamba
hali hiyo ikiendelea hivyo miaka 50 ijayo Tanzania haitakuwa kisiwa cha amani
tena.Walitoa kauli hiyo kwenye kongamano
lililofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuhusu mustakabali wa amani na
usalama wa taifa letu miaka 50 ijayo
. Walidai kuwa jinsi Serikali inavyotumia
vyombo vyake vya dola kukandamiza wananchi wana imani miaka 50 ijayo amani
haitakuwepo nchini.Mmoja wa wanasheria, Lilian Wassira,
alisema kinachoponza Watanzania ni woga kiasi cha kuwafanya washindwe kudai
haki zao. "Watanzania wasingekuwa woga wangeibana Serikali hadi kuiondoa
madarakani," alisema. Kuhusu vikundi vya ukakamavu, alisema haoni shida
kila chama kuwa na vikundi hivyo.
"Mbona vyama vingine vinavyo, wao
wanahofia nini?" Alihoji. Kwa upande wake mbunge wa CHADEMA, Tundu Lissu,
alisema pamoja na Tanzania kuitwa kisiwa cha amani, lakini yeye anaiona kama
kisiwa cha ukandamizaji.Alitoa mfano kuwa mwaka 1967 wakati wa
kuanzisha vijiji vya ujamaa kuna watu waliwekwa ndani. Alisema kuwa hata mwaka
1980 kuna watu waliwekwa ndani walipohoji uhalali wa Muungano. Lissu alisema
kwenye miaka ya 1980 kuna watu waliondolewa kwenye vijiji vyao ili kupisha
uchimbaji wa madini.
Alisema anawashangaa wasomi
kutozungumzia masuala hayo badala yake wamejikita kwenye suala la ajira. Kwa
upande wa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Willbrod Slaa, alisema anamshangaa Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi (Dkt. Emmanuel Nchimbi) kutojiuzulu wakati jeshi la
polisi linaongoza kwa kuvunja haki za wananchi.
Alitoa mfano mauaji ya mwandishi wa
habari, Daud Mwangosi, kuwa hadi sasa hakuna ripoti iliyotolewa huku twiga
wakiibwa na kusindikizwa na askari. Alisema Mtwara kuna uvunjifu wa amani na
wanaofanya hivyo ni vyombo vya dola."Chanzo cha kupotea kwa amani
itakuwa ni jeshi la polisi," alisema. Naye Profesa Mpangala, alisema chama
tawala kisipojiondoa kwenye dola miaka 50 ijayo Tanzania haitakuwa tena kisiwa
cha amani.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro, anasema
tunapoelekea Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linaelekea kupoteza
sifa. Alitoa mfano kuwa viongozi wa chama hicho walipigwa na JWTZ, lakini
hakuna hatua zilizochukuliwa
No comments:
Post a Comment