Na Goodluck
Hongo
KAMATI ya Vijana Wapenda Ama n i Ta n z
a n i a (KVT ) ime w a t a k a Wa t a n z a n i a kujihadhari na watu wanaotaka
urais kupitia vyombo vya habari, makanisani na misikitini kwani watakapoingia
madarakani ni rahisi kuvuruga amani ya nchi kwa kutekeleza yale ya upande mmoja
na kuacha mwingine.
Akizungumza na
waandishi wa habari Dar es Salaam
jana Mwenyekiti wa KVT, Chifu Msopa, alisema hali ya kisiasa kwa sasa si nzuri
na kuna hatari kuwapitisha viongozi wanaopita makanisani na misikitini, wale
wenye nia ya kulipa visasi.
Kamati hiyo
inajumuisha vijana kutoka katika vyama vyote na dini kutoka mikoa yote nchini.Alisema wao
wakiwa kama viongozi wana wajibu wa kusema
pale ambapo hali inaenda vibaya kutoka kwa wale wanaojitosa kwenye mbio za
kuwania urais.Alisema taasisi
hiyo imejadili kwa kina vijana kupendekezo wanaofaa kuwania nafasi hiyo na
kutokana na kuwa na sifa nzuri.
"Kwa
upande wa vijana tumeona watu wenyewe sifa za kugombea urais ni wanne tu,"
alisema.Aliwataja
vijana wanaofaa kuwania urais kuwa ni Zitto Kabwe, James Mbatia,January Makamba
na Dkt.Hussein Mwinyi. Alisema sifa kubwa z a wa t u h a o n i we n y e
maadili,hawana chuki wala visasi ndani ya vyama vyao na nje ya vyma vyao.
"Lakini
pia si viongozi wababe wala hawana chembechembe za udikteta na uongozi wa kiimla,
ni viongozi ambao wanawaunganisha Watanzania kwa dini zao makabila yao kanda
zao pande zao,"alisema.
Alibainisha
kuwa wao kama kamati ya vijana wamegundua kuwa watu wamekuwa na visasi na
kuonya kuwa kama atachaguliwa mtu ambaye anapita makanisani na misikitini na
baada ya kupata urais akashindwa kulipa fadhila kwa Wakristu au Waislamu
atasababisha migogoro.Aliongeza kuwa,
kama vyama vyao vitateua majina ya wanasiasa hao vijana taasisi hiyo itakuwa
wapo tayari kuzunguka nchi nzima kuwapigia debe ili washinde urais.
Naye Katibu
Mkuu wa Kamati hiyo, Sadiki Godigodi, alisema taasisi hiyo ina vijana kutoka
pande zote za nchi na kazi yake ni kuhimiza amani, upendo, umoja na mshikamano
miongoni mwa Watanzania. Alisema kazi yake nyingine ni kuhimiza vijana
kujitolea.
Alisema japo
kwa sasa si njia sahihi ya kujadili majina ya wagombea urais, lakini nyufa
alizowahi kusema Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julias Nyerere zimeanza
kuonekana, ikiwemo chuki kati ya viongozi wa kisiasa walio ndani ya chama
kimoja, kuongezeka uadui wa kisiasa baina ya vyama vya siasa,kushuka vya
ufanisi na weledi katika taasisi muhimu kama bunge, mahakama na polisi.
"Katika nchi inayohitaji mabadiliko kama
nchi yetu uzoefu wa miaka mingi wa siasa si kipimo kizuri cha uongozi bora kwani
kwa sasa nchi hii haihitaji uzoefu wa siasa ila kinachotakiwa ni kwamba ili
chama kishinde kinapaswa kuteua mgombea anayeshabihiana na Watanzania walio
wengi ambao ni vijana," alisema Godigodi
No comments:
Post a Comment