03 July 2013

WASANII WA BONGO MUVI WAITEKA MWANZA


 Na Mwandishi Wetu, Mwanza
WAKAZI wa Mwanza na vitongoji vyake juzi walishuhudia vitu tofauti wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Filamu la Wazi la Grand Malt Tanzania, ulioongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya, lililofanyika kwenye Uwanja wa Nyamagana, jijini hapa.
Tamasha hilo maarufu kama 'Grand Malt Tanzania Open Film Festival' lilinogeshwa zaidi na burudani kali kutoka kwa bendi ya Extra Bongo, waliokuwa wakiongozwa na Ally Choki.

Shamrashamra za uzinduzi huo zilionekana toka mapema alfajiri, wakati wasanii wa Bongo Movie walipojikuta wakibanwa kila mahali walipokuwa wakipita kutambulisha ujio wao.
Wakati wa uzinduzi huo, wasanii waliokuwepo uwanjani hapo wakiongozwa na Hashima Kambi, walijikuta wakizongwa kwa muda wote, huku mashabiki wakitaka kuwashika au kupiga nao picha.
Aunty Ezekil, Irene Uwoya, Jacqueline Wolper, Vicent Kigosi 'Ray' na Jacob Steven 'JB' walijikuta wakishangiliwa muda wote kama ilivyokuwa kwa Hashim Kambi, Isa Musa 'Cloud' na Steve Nyerere.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya, alisema amefurahishwa mno na tamasha hilo na hasa watu waliokuwa wamejitokeza kwa wingi kushuhudia wasanii wao.
"Serikali itaendelea kuthamini kwa kiasi kikubwa wasanii wetu na huu ni wakati wa wasanii wa Mwanza kujifunza kutoka kwa mastaa wetu hawa," alisema.
Meneja wa kinywaji cha Grand Malt, Consolata Adam alisema, wameamua kulidhamini tamasha hilo kwani wanajua watu wengi kwa sasa wanapenda kutazama filamu za Tanzania.

No comments:

Post a Comment