BAADHI ya wanawake katika Kata ya
Pasua, Manispaa ya Moshi wametaka mabaraza ya katiba kuweka vipengele
vinavyoainisha mirathi, haki za wanandoa na watoto mara baada ya ndoa kuvunjika
na mmoja au wote wanapofariki.Wanawake hao
Mwanvita Kishe na Lillian Mwendani walisema hayo katika mdahalo wa usawa wa
kijinsia ulioandaliwa na asasi ya mazingira mkoani Kilimanjaro (KENOT) kwa
ufadhili wa The Foundation For Civil Society na kufanyika mjini humo.
Walisema ombi
hilo linatokana na unyanyasaji wanaopata wanawake, watoto wanaozaliwa kabla,
baada ya ndoa kuvunjika na wale wanaotelekezwa kutokana na matukio hayo
kukithiri katika siku za hivi karibuni."Kwa kuwa
katiba ndiyo sheria mama ipo haja kuainisha baadhi ya masuala ambayo yamekuwa kikwazo
kwa wanawake wajane na watoto wote bila kujali amezaliwa kabla au baada ya
ndoa," alisema Massawe
Alisema kuna
baadhi ya sheria zikiwemo za ustawi wa jamii na zile za ndoa ambazo hazitoi
haki sawa baada ya watu kuchuma kwa pamoja na badala yake wanawake wamekuwa
wakiteseka na watoto wanaoachiwa.Awali
akichangia katika mdahalo huo Ustadhi Marimbo Mmbaga aliziomba asasi hizo na
viongozi wengine wa dini kusaidia kutoa elimu sahihi juu ya usawa wa kijinsia
ili kuepusha upotoshaji unaofanyika.
Alisema usawa
wa kijinsi unapaswa kuandamana na kusaidiana katika majukumu ya kila siku, haki
na wajibu katika jamii na sio kama inavyotafsiriwa na baadhi ya watu na kukataa
kufanya kazi.Kwa upande wake Mwenyekiti wa KENOT, Rodrick Maimu alisema suala la haki
sawa linahitaji elimu na muda zaidi wa kuirekebisha jamii kwani kutokana na
mfumo wa hapo awali mwanamke alionekana kutokuwa na thamani kabisa
No comments:
Post a Comment