Na John
Gagarini, Kibaha
MKAZI wa Kijiji cha Nyanduturu Wilaya ya
Mkuranga Mkoa wa Pwani, Ally Makakatau (46), amefariki baada ya kuvamiwa
nyumbani kwake na kukatwa na mapanga na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.Kwa
mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Juma Ally alisema kuwa tukio
hilo lilitokea Julai 19 saa 7:30 usiku baada ya watu wapatao sita kuvamia
nyumbani kwa Makakatau na kuvunja mlango wa nyumba aliyokuwemo kisha
kumshambulia kwa kutumia mapanga kichwani, mkononi na miguuni.
Ally
alisema kuwa watu hao walivamia katika nyumba hiyo na kumtaka marehemu
kuwapatia fedha ambazo alikuwa amepata baada ya mauzo ya mafuta aliyokuwa
amefanya jioni ya siku hiyo na alipokataa kutoa ndipo waliamua kumkata kwa
mapanga sehemu mbalimbali za mwili."Watu hao mbali
ya kuvunja nyumba ya mfanyabiashara huyo, pia walivunja duka na kuchukua pesa
taslimu shilingi m 2,800,000 ambazo zilikuwa ni za mauzo ya mafuta,"
alisema Ally.
Aliongeza kuwa Jeshi
la Polisi linawasaka watu hao na kuwataka wananchi kuwapatia taarifa zitakazo
saidia kuweza kuwapata waliohusika na tukio hilo.Aidha alisema kuwa
mwili wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi wa daktari na tayari umekabidhiwa kwa
ndugu wa marehemu kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Katika tukio lingine,
Polisi Mkoa wa Pwani inawashikilia watu 20 raia wa Ethiopia kwa kosa la kuingia
nchi bila kibali.
Alisema kuwa tukio
hilo lilitokea saa 7:30 usiku eneo la Mkuranga Mjini Wilaya ya Mkuranga.Kamanda huyo
alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa watu hao walikamatwa na
askari waliokuwa doria wakiwa wanatembea kwa makundi katika eneo la Mkuranga
Mjini.
Alifafanua kuwa watu
hao baada ya kuwahoji walibaini kuwa walishushwa kwa gari na kuamua kutembea
ili kuweza kuvuka kwenye eneo lililokuwa na kizuizi cha polisi.Aidha, aliwataka wananchi waendelee
kutoa taarifa kwa polisi pindi wanapowatilia mashaka wageni wanaoingia kwenye
maeneo yao.
No comments:
Post a Comment