26 July 2013

WANASIASA WAVURUGA KAMPENI YA USAFI ARUSHA



Na Queen Lema, Arusha
MWENYEKITI kamati ya usafi Mkoa wa Arusha, Adolf Ulomi amesema kuwa kampeni ya usafi wa Jiji la Arusha bado inakabiliwa na changamoto kubwa hasa ya baadhi ya wanasiasa kuingiza siasa kwenye suala hilo jambo ambalo wakati mwingine linafanya jiji kuonekana bado chafu.

Ulomi aliyasema hayo jana katika eneo la Kwa Muorombo wakati Kamati hiyo ikiendelea na usafi wa Jiji na kuhusisha wananchi pamoja na wafanyabiashara wa eneo hilo. Alisema kuwa pamoja na kuwa kamati hiyo ya usafi imejizatiti katika kuhakikisha kuwa Jiji la Arusha linakuwa safi lakini baadhi ya wanasiasa wa Mkoa wa Arusha wanatumia vyeo vyao kupotosha maana halisi ya Kamati hiyo lakini pia umuhimu wa jiji kuwa safi.
Alifafanua kuwa baadhi ya wanasiasa hao mara nyingine wanadai kuwa wanawaonea huruma wananchi hasa wale ambao wanaharibu mazingira huku baadhi ya wananchi hao nao wakitumia muda huo kuchafua mazingira kwa kisingizio kuwa wamepewa ruhusa na wanasiasa wao.
P i a a l i s ema wa n a s i s a s a wanatakiwa kuiga mfano wa usafi kwenye miji mingine ambayo imeendelea duniani na hata baadhi ya miji hapa nchini ukiwemo mji wa Moshi jinsi ambavyo wameungana na kisha kuwabana baadhi ya wananchi wanaochafua mazingira jambo ambalo limekubalika na limejengeka kuwa usafi ni wa jamii na wala sio wa Serikali.
Wakati huohuo aliishauri Serikali kuwa inatakiwa kuwa bunifu zaidi kwenye sekta ya uwekezaji kwani kama sekta hiyo ikiwa ni kubwa hata wafanyabiashara wadogowadogo ambao wakati mwingine wanauza bidhaa zao bila kujali usafi wa mji wataweza kuwa na ajira.
Ulomi alifafanua kuwa kwa sasa katika mji wa Arusha asilimia kubwa ya wafanyabiashara wadogo wamesambaa kila kona lakini kama kungekuwa na fursa za uwekezaji basi wangezitumia vyema hivyo hata usafi ungeimarika zaidi.

No comments:

Post a Comment