Na
Mwajuma Juma, Zanzibar
WAJUMBE wa Baraza la Katiba wa Wilaya ya Mjini wamesema kuwa kuendelea
kuwepo kwa sarafu moja na Benki Kuu moja katika mambo ya Muungano ni kuumiza
sehemu moja kiuchumi. Wakizungumza
katika mkutano wa baraza hilo uliofanyika mjini Unguja wajumbe hao walisema
kuwa uchumi wa nchi hizo mbili ni tofauti kutokana na Zanzibar uchumi wake ni
huduma na Tanganyika ni wa rasilimali ambao hauwezi kulinganishwa na uchumi wa
Zanzibar.
"Zanzibar uchumi wake ni huduma, Tanganyika ni wa rasilimali hivyo kuendelea kuwa na Benki Kuu moja ni kuumiza sehemu moja ya Muungano hasa Zanzibar ambayo uchumi wake ni wa huduma," alisema mjumbe kutoka Shehiya ya Malindi Mustafa Bakari Sharif.
Alisema
kuwa imefika wakati sasa kila nchi iweze kusimamia masuala yake yenyewe ya nchi
ili kuweza kuendesha nchi yake kitaifa na kimataifa. Kuhusu
masuala ya nje alisema kuwa kuwepo kwake katika orodha ya Muungano ni
kuzikosesha nafasi nchi mbili hizo kutambulika kimataifa, hivyo ni vyema
wakaachiwa kila nchi iendeshe nchi yake kimataifa.
Nae
Firdausi Abdulrahman alisema kuwa rasimu iliyopo ya kutengeneza katiba mpya
haioneshi kutambua ushirikiano pamoja na nembo ya Taifa kutoonesha sura ya
ushirikiano wao.
Sambamba
na hilo alisema kuwa ipo haja ya kuanzishwa
utaratibu maalumu wa uingiaji wa watu ili kuepusha kujitokeza ongezeko la watu
hasa
Mambo yote saba yaliyopendekezwa na tume yawe ya muungano bado si suluhisho la kuifanya nchi kuwa na mamlaka kamili.
ReplyDeleteHoja za msingi zilizotolewa hapa zinapaswa ziangaliwe upya na tume ya mabadiliko ya katiba.
inapaswa kwanza kuundwa katiba ya Tanganyika na ile ya watu wa Zanzibar kisha yawepo majadiliano ya kipi kiingizwe kwenye muungano ambacho hataumiza upande wowote.