Na Martha Fataely, Mwanga
WAKAZI wa Kijiji cha
Uchira wameomba s u a l a l a ma v a z i kuwekwa kisheria ili kukabiliana na
ukiukwaji wa maadili unaofanywa sasa na baadhi ya wanawake na wanaume na
kuchangia kuwapo kwa maambukizi mapya ya Ukimwi.
Kutokana na hilo,
wameomba ziwekwe sheria ndogo ndogo ambazo zitakuwa zikitoa adhabu zikiwamo
faini kwa wale wote watakaozikiuka na hivyo kupotosha maadili kwa kizazi
kijacho.
Wakizungumza wakati wa mdahalo wa usawa wa kijinsia ulioandaliwa na
Shirika la Mazingira mkoani Kilimanjaro (KENOT) kwa ufadhili wa The Foundation
for Civil Society, Theresia Msuya na Ajenta Lyimo wamesema itasaidia kulinda
utu.
"Jinsi mavazi yanavyovaliwa sasa, ipo haja kwa halmashauri za
wilaya na manispaa kwa kushirikiana na serikali, kuunda sheria hizo ambazo
zitalinda maadili, lakini pia kupunguza matamanio ya kushiriki ngono
yanayochangiwa na mavazi," alisema.
Katika hatua nyingine baadhi ya wauguzi kwa kushirikiana na ndugu
wa wagonjwa wamedaiwa kuwafanyia ukeketaji wanawake wa j awa z i t o wa k a t i
wa kujifungua na hivyo kuwaathiri kisaikolojia.
Akizungumza wakati wa mdahalo huo, Mjumbe wa KENOT, Josephine
Mfaume a l i s ema v i t e n d o h i v y o vimeshamiri zaidi katika wilaya ya
Rombo huku wanawake husika wakibaini kufanyiwa hivyo hutakiwa kutunza siri
vingine hutengwa na ukoo.
Aidha alisema kuwa ushuhuda wa kufanyika kwa vitendo hivyo pia
ulitajwa katika siku 16 za kupinga ukatili ambapo baadhi ya wanawake wa wilaya
hiyo walielezea na kuomba ushauri na msaada wa kisheria ili kukomesha vitendo
hivyo.
Hata hivyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dkt. Faisal Issa
alikanusha kuwapo kwa madai hayo lakini akaahidi kufuatilia ili kama kuna
ukweli wahusika wasakwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Pamoja na kauli hiyo lakini katibu wa hospitali ya mkoa huo,
Boniface Lyimo alikiri kusikia malalamiko hayo ambayo hata hivyo alidai
hayakuwa na uthibitisho ingawa juhudi za kufanyia uchunguzi zimeanza
No comments:
Post a Comment