30 July 2013

WAKULIMA WAHADHARSHWA KUIBUKA UKAME



 Chamacha Wakulima Tanganyika (TFA) kimesema kuwa wananchi wa Kanda ya Kaskazini wanatakiwa kujiwekea akiba ya vyakula kwani mikoa hiyo huenda ikakabiliwa na ukame mkubwa kutokana na baadhi ya wakulima kukosa pembejeo za msingi huku wengine mpaka sasa mazao yao yakiwa yamedumaa mashambani, anaripoti Queen Lema, Arusha.

Hata hivyo, kwa kipindi hiki Kanda hiyo ya Kaskazini itakabiliwa na kiwango cha zaidi ya asilimia 40 cha ukame tofauti na msimu wa mavuno wa mwaka jana ambacho kilikuwa chini ya asilimia hizo.
Ha y o y a l i e l e zwa n a Mwenyekiti wa chama hicho, Elias Mshiu wakati akizungumza kwenye mkutano wa 56 wa chama hicho uliofanyika katika eneo la TFA Shoprite Jijini Arusha mapema jana.
Ms h i u a l i s ema k uwa tahadhari hiyo inapaswa hata kuchukuliwa na jamii yote ya Kanda ya Kaskazini kwani mpaka sasa baadhi ya maeneo hayana mazao kabisa hali ambayo wakati mwingine inaashiria baa la njaa kwa msimu ujao wa chakula.
Akielezea chanzo kikubwa cha wakulima wengi kukosa mazao kwa msimu ujao wa mavuno alisema kuwa sababu kubwa kabisa ni ukosefu wa pembejeo za kilimo kwa wakati kwani toka msimu wa kulima na kupanda bado zilikuwa hazijafika na hatimaye baada ya zoezi la upandaji ndipo pembejeo hizo zilipofika,
Aliongeza kuwa hali hiyo ilisababisha baadhi ya wakulima kulima, kupanda bila pembejo ikiwemo mbolea jambo ambalo limesababisha baadhi ya mashamba kukosa mazao lakini pia hata yale ambayo yametoka nayo hatyaridhishi kwa matumizi ya chakula na biashara.
"Tahadhari kubwa inatakiwa kuchukuliwa kwani msimu ujao wa mavuno haki itakuwa ni tete sana na sasa huenda mikao hii ya kaskazini ikakumbwa na njaa kali kuliko ile ya mwaka jana lakini pia kama tahadhari itachukuliwa mapema itasaidia hata kuweka akiba hususani kwenye familia zile ambazo hazina uwezo," aliongeza Mshiu.
Awali, alisema kuwa kwa sasa hata kilimo cha Kanda ya Kaskazini bado kinakabiliwa na changamoto kubwa sana kwani baadhi ya wakulima wanategemea zaidi majira ya mwaka huku hali hiyo ikisababisha wengi kukosa mazao
Mshiu aliongeza kuwa kama uwekezaji mkubwa utawekwa kwenye kilimo cha umwagiliaji basi kanda ya kaskazini itakuwa ni miongoni mwa kanda zenye vyakula vya kutosha kwa ajili ya matumizi ya vyakula, lakini pia kwa ajili ya biashara.
Katika hatua nyingine, wakulima wa chama hicho waliiomba Serikali na wadau wengine wa kilimo kuweka mikakati mbalimbali ambayo itaweza kuboresha zaidi kilimo cha umwagiliaji kwani aina ya kilimo ambacho kinafanyika kwa sasa cha kutegemea zaidi majira ya mwaka ni cha kubahatisha kwani kilimo cha umwagiliaji ni cha majira yote ya mwaka.  

No comments:

Post a Comment