29 July 2013

WANAFUNZI HATARINI KUKUMBWA NA MAGONJWA



 Na Mashaka Mhando, Tanga
WAZAZ I wa wa t o t o wanaosoma katika Shule ya Msingi Azimio iliyopo Kata ya Makorola katika Jiji la Tanga, wameonesha wasiwasi wao wa kutokea magonjwa ya mlipuko kutokana na shule hiyo kukosa vyoo kwa matuminzi ya wanafunzi.

Mmoja wa wazazi waliokuwa na watoto wanaosoma katika shule hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Papaa Bokande, alisema shule hiyo imekuwa haina maji, vyoo na mlinzi licha ya wazazi kutoa michango kila mwezi kuchangia gharama hizo.
"Kwa kweli tunasikitika watoto wetu wanasoma katika shule ambayo haina vyoo, maji na mlinzi, tuna wasiwasi kunaweza kutokea magonjwa ya mlipuko pale ni hatari sana na sisi tumekuwa tukichanga fedha kila mwezi," alisema Bokande.
Alisema mwezi uliopita walifanya kikao na mwalimu mkuu wa shule hiyo aliyemtaja kwa jina moja la Mndolwa ambapo walikubaliana kuishinikiza halmashuari ya jiji kujenga vyoo kwa ajili ya kuokoa watoto wao lakini wanaona kama suala hilo halishughulikiwi.
Mwandishi wa habari hizi alipofika shuleni hapo mwishoni mwa wiki, hakuweza kumkuta Mkuu huyo wa shule ambapo mmoja wa walimu aliyekutwa hapo alisema mkuu wao amekwenda halmashauri ya Jiji kwenye vikao vyao vya mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo, mwalimu huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini, alisema kuwa shule hiyo iliyoanzishwa miaka sita iliyopita, inatumia vyoo vya shule mama iliyopo jirani na shule hiyo ya Makorola ambayo wanafunzi wote wanatumia vyoo hivyo.
"Mwalimu Mkuu hayupo amekwenda ofisi za Jiji, lakini suala hilo la shule kukosa vyoo si kweli wanafunzi wanatumia vyoo vya shule mama ya Makorola lakini mpango wa kuchimba vyoo upo ni utekelezaji tu wa suala hili," alisema mwalimu huyo.

No comments:

Post a Comment