29 July 2013

WAKULIMA WAWEZESHWA KUHAKIKI UBORA WA KAHAWA



 Na Florah Temba, Moshi
WAKUL IMA 1 , 0 0 0 wa kahawa katika wilaya sita za Mkoa wa Kilimanjaro na Arumeru mkoani Arusha, wanatarajia kunufaika na mradi wa kuwajengea uwezo juu ya usajili na uhakiki wa kahawa yenye ubora lengo likiwa ni kuwawezesha kutekeleza mbinu bora za kilimo endelevu na kujikwamua kiuchumi. Mradi huo wa kuwajengea uwezo wakulima wa kahawa juu ya usajili na uhakiki wa kahawa yenye ubora katika nchi wanachama wa Shirika la Kahawa Mashariki mwa Afrika (EAFCA) ulianza kutekelezwa kwa ufanisi nchini Tanzania Julai 2011 ambapo utamalizika mwaka 2015 na unatarajiwa kuwafikia wakulima zaidi ya 1,000.

Akizungumza mwishoni mwa wiki wakati wa kutolewa mafunzo kwa wanachama zaidi ya 40 wa chama cha msingi cha Kibong'oto Wanri, mtafiti wa usambazaji teknolojia na mafunzo katika taasisi ya utafiti wa kahawa Tanzania (TaCRI), Jeremiah Magesa alisema taasisi hiyo inawajengea wakulima uwezo na kuwatafutia soko la uhakika la kahawa.
Alisema lengo hasa la mradi huo ni kuwawezesha wakulima kuzalisha kahawa yenye ubora ambayo itakubalika katika soko hali ambayo itawawezesha kuongeza kipato na kuondokana na lindi la umaskini. "Wakulima 1,000 katika wilaya za Rombo, Hai, Siha, Mwanga, Moshi vijijini, Same mkoani Kilimanjaro na wilaya ya Arumeru mkoani Arusha watafundishwa juu ya usajili na uhakiki ili kukidhi vigezo vinavyohitajika katika soko, kutokana na ukweli kwamba soko la kahawa kwa sasa linaangalia ubora," alisema Magesa.
Kwa upande wao baadhi ya wakulima wa kahawa Kibong'oto Wanri waliipongeza taasisi ya TaCRI kwa kuwapatia mafunzo hayo na kusema kuwa yamewawezesha kujitambua na kuzingatia kanuni bora za kilimo cha kahawa hali ambayo wanaamini itawawezesha kuingia kwenye ushindani wa soko la kahawa la kitaifa na la kimataifa. Amini Munuo alisema wakulima wengi wamejisahau na kuendeleza kilimo cha zamani kisicho na tija hali ambayo imewafanya kukosa soko la uhakika na kuathirika kimapato.
Alisema mafunzo hayo waliyopewa ni msaada mkubwa kwao katika kuhakikisha wanaboresha kilimo cha kahawa na kuzalisha kahawa bora ambayo itakubalika katika masoko ya kimataifa na hatimaye kuongeza kipato na kupiga vita adui umaskini.
Naye Meneja wa Mradi huo Afrika, Filtone Sandando alisema wanahitaji vizazi vijavyo vinufaike na mradi huo na kuhakikisha wanazalisha kahawa bora ambayo itawawezesha kuongeza kipato chao. A l i s e m a w a m e l e n g a kuwasaidia wakulima kupata bei nzuri ya kahawa pindi watakapozingatia kanuni za kilimo bora cha kahawa hatua ambayo itawawezesha kujikwamua kiuchumi

No comments:

Post a Comment