03 July 2013

VITAL'O YATWAA UBINGWA KAGAME


Na Mwandishi Wetu
TIMU ya Vital'O ya Burundi juzi usiku ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Afrika Mashariki na Kati maarufu kama Kagame baada ya kuifunga APR ya Rwanda mabao 2-0.
Mechi hiyo iliyokuwa na upinzani mkali ilichezwa Uwanja wa El Fasher Jimbo la Darfur Kaskazini nchini Sudan.
Waliokuwa mashujaa wa Vital'O ni Amisi Tambwe aliyefunga bao dakika ya 63 na Deo Ndayishimiye ambaye alifunga dakika ya 65.
Vital'O chini ya kocha wake mpya Mnyarwanda Yaounde Kanyankore ilifanikiwa kutawala mchezo na kuidhibiti ipasavyo APR ambao walitaka kuchukua kombe hilo lililopachikwa jina la Rais wao Paul Kagame, lakini ngome ya Warundi hao ilikuwa imara.
Mwaka jana Yanga ndio waliokuwa mabingwa wa kombe hilo, lakini mwaka huu timu za Tanzania hazikushir
iki michuano hiyo kwa kuhofia hali ya usalama nchini Sudan.

Katika michuano hiyo bingwa ambao ni Vital'O waliondoka na kitita cha dola za Marekani 30,000, washindi wa pili APR ya Rwanda dola 20,000 na mshindi wa pili ni wenyeji El Merreikh walishika nafasi ya tatu na kupata dola 10,000, wenyeji hao
Na Mosi Mrisho
MBIO za kuwania madaraka ndani ya Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), zimeanza na zinatarajiwa kuhitimishwa jijini Mwanza kesho ambapo uchaguzi huo utafanyika.
Akizunmgumza Dar es Salaam jana Afisa Michezo Msaidizi wa BFT Richard Mganga, alisema mpaka sasa wamejitokeza watu watano kuchukua fomu za kuwania uongozi ndani ya chama hicho.
Maganga alisema uchaguzi huo utafanyika baada ya viongozi wa sasa kumaliza muda wao wa uongozi kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.
Alisema wapo watu wengi wanaohitaji kuingia kwenye uongozi huo, lakini zipo sifa mbalimbali ambazo zinahitajika ili kuweza kushiriki uchaguzi huo.
Maganga aliongeza kuwa wadau kabla ya kufikiria kuingia BFT lazima wagombea wajichuje wenyewe, ambapo mgombea pamoja na elimu yake au kuwa na sifa nyengine anatakiwa kuwa na sifa za uongozi nauzoefu wakutosha.
Alisema mpaka sasa waliojitokeza kuchukua fomu za kuomba uongozi ni watano.

No comments:

Post a Comment