03 July 2013

MICHUANO AIRTEL RISING STARS TAIFA YAANZA DAR


 Na Mwandishi Wetu
TIMU y a Ki n o n d o n i wasichana imeanza vizuri michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars 2013 ngazi ya Taifa, kwa kuwafunga mahasimu wao timu ya Ilala 2-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam jana.
Kinondoni waliuanza mchezo huo kwa kasi mara tu baada ya kipenga cha kwanza kupulizwa na juhudi zao zilizaa matunda dakika ya tano wakati mchezaji Anna Ebron alipoachia shuti la mbali na kwenda moja kwa moja wavuni na kumuacha mlinda mlango wa timu ya Ilala akichupa bila mafanikio.

Goli hilo liliamsha hamasa kutoka kwa mashabiki wa Kinondoni.
Baada ya hapo Ilala walianzisha mashambulizi na kulisakama lango la wapinzani wao kwa lengo la kupata goli la kusawazisha lakini walinzi wa timu ya Kinondoni wa l i k uwa ma k i n i k u o k o a mashambulizi hayo.
Kwa u j uml a Ki n o n d o n i walionesha mchezo mzuri na pengine wanaweza kutimiza ndoto yao ya kutwaa kombe ya ARS upande wa wasichana mwaka huu.
Timu zote zilianza kipindi cha pili kwa ari mpya na kupata nafasi kadhaa za kufunga na ilikuwa ni Kinondoni tena waliofanikiwa kupata goli katika dakika ya 56 kupitia kwa Rehema Yahya baada ya kupata krosi kutoka upande wa kulia na kufunga goli la pili.
Mechi hiyo ilifuatiwa na mchezo mwingine kati ya Kinondoni na Temeke wavulana ambapo Kinondoni ilishinda 2-1. Mchezo huo ulikuwa mkali na ulivuta hisia za wapenzi na wadau wengi wa soka akiwemo kocha wa timu ya taifa ya vijana Jacob Michelsen ambaye alisifu kiwango cha mchezo kilichooneshwa na timu hizo.
"Nafikiri michezo hii itatoa fursa nzuri ya kubaini vipaji vya wachezaji chipukizi na kusema kweli itatusaidia kupata timu ya vijana ya Taifa chini ya umri wa miaka 17 ambayo tutaiunda hivi karibuni," alisema Michelsen baada ya kushuhudia mechi hizo za mwanzo.
Katika mchezo wa wavulana Kinondoni walikuwa wa kwanza kutikisa goli la wapinzani wao wakati mchezaji machachali Mustafa Yusuf alipopata krosi kutoka upande wa kulia na kuunganisha mpira wavuni kwa shuti kali.
Goli hili lilibadili kasi ya mchezo huku Temeke wakishambulia kwa nguvu na kufanikiwa kupata goli la kusawazisha dakika ya 28 kupitia kwa Salum Issa.
Kipindi cha pili Kinondoni waliutawala mchezo kwa kosa kosa nyingi na alikuwa Willy Kalolo aliyewainua washabiki wa timu hiyo baada ya walinzi wa Temeke kufanya uzembe na kumuwezesha mfungaji kupata mpira kwa urahisi katika eneo la hatari na kufunga goli la kuongoza katika dakika ya 50.
Mashindano ya Airtel Rising Stars mwaka huu yanashirikisha timu kutoka mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni, Temeke (wasichana na wavulana), Mwanza, Morogoro, Mbeya (wavulana), Tanga, Ruvuma na Kigoma (wasichana).
Timu ziliwasili jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na kufanyiwa uhakiki wa umri tayari kwa mashindano ya ngazi ya Taifa ambayo yalitarajiwa kufunguliwa rasmi na Naibu Waziri Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Kassim Majaliwa.

No comments:

Post a Comment