Na
Ignas Andrew
MW E N Y E K I T I wa Ch ama c h a
Wananchi(CUF) W i l a y a y a Kinondoni, Juma Nkumbi amesema serikali inatakiwa
kuwanyonga viongozi wanaohusika na mtandao wa dawa za kulevya ili iwe fundisho.
Hayo aliyasema jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini
Dar es Salaam kuhusiana na mwenendo mzima wa mmong'onyoko wa maadili wa vijana
ambao ndio nguvukazi ya Taifa lijalo.
Akizungumza na jana, mwenyekiti huyo ambaye pia ni diwani wa kata ya
Kibada wilaya ya Temeke, alisema kuwa, Taifa linaendelea kumong'onyoka
kimaadili kwa kuwa uwajibikaji wa serikali ni kimazoea; hivyo ameitaka
kuhakikisha anatumia sera ya nchi ya China kwa kuanza kunyonga viongozi wote
wanaohusika.
"Uwajibikaji huu wa kimazoea ndio unaomaliza Taifa,wakati vitu vipo
wazi sidhani kama kweli serikali haifahamu wanaoyaingiza madawa hayo,lakini
hakuna hatua zinazochukuliwa kwa kuwa pamekuwapo na rushwa; na urafiki,"
alisema Nkumbi.
Wa k a t i h u o h u o ; mwenyekiti huyo
ameyataka mabaraza ya kaya ya katiba kuhakikisha wanaipitia ipasavyo rasimu
mpya ya Katiba ili kutoa maoni ambayo yanatachangia kupata kanuni na sheri
bora.
"Wajumbe wa mabaraza ya katiba hakikisheni mnaipitia vizuri katiba
kwanza,kabla ya kuitolea maamuzi,na maoni ili tupate miongozo sahihi ambayo
itatumika kama kanuni za utawala bora,badala ya kuwa na bora utawala,"
alisema Nkumbi.
Alisema kuwa
inasikitisha mno kuona jamii inaendelea kupoteza nguvukazi ya Taifa ambayo
inaangamia kwa matumizi ya dawa za kulevya kwa sababu ya manufaa ya watu
wachache ambao wametazama na kujali maisha yao na kulitupa Taifa.
Aidha, kwa
upande mwingine Mwenyekiti huyo amelaani vikali vitendo vinavyofanywa na mamlaka
ya Dawa na Chakula nchini (TFDA) kwa kuidhinisha matumizi ya dawa zisizofaa kwa
jamii.
"Lingine
ambalo nalipigia kelele hivi ni kweli Mamlaka ya Dawa na Chakula inawezaje
kupitisha dawa zisizofaa,hali ambayo inapelekea jamii ya Watanzania kupoteza
uhai halafu bado Serikali inatazama tu?" alihoji mwenyekiti huyo.
No comments:
Post a Comment