15 July 2013

ANYEDAIWA KUKUTWA NA VIUNGO VYA BINADAMU AACHIWA


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi wilayani Handeni, imemwachia huru Mkazi mmoja wa Kijiji cha Kwamnele kilichopo Kata ya Ndolwa, Mohamed Rajab (38) ambaye alikuwa akikabiliwa na shtaka la kukutwa na viungo vya binadamu kinyume cha sheria.
Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, Patrick Maligana, alisema kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani hapo haukuwa wa moja kwa moja wa kuweza kumtia hatiani mshtakiwa.
Alisema mashahidi wa tukio hilo walitoa ushahidi ambao hauwezi k u t h i b i t i s h a k u w a mtuhumiwa anahusika na tukio hilo kwa kueleza mambo tofauti, hivyo mahakama inamwachia huru mtuhumiwa na rufaa kwa washtaki ipo wazi.

Awali, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Nzagalila Kikwelele alidai mahakamani hapo kwamba mnamo Machi 2 mwaka 2011 mtuhumiwa huyo alikamatwa kwa kosa la kukutwa na viungo vya binadamu nyumbani kwake.
A l i s e m a katika upekuzi u l i o f a n y w a chumbani kwake alikutwa na fuvu la binadamu, taya na mifupa ya mbavu vikiwa vimefukiwa nyuma ya nyumba yake huku pembeni ya eneo hilo kukiwa na sanda.
Hata hivyo, alipotakiwa kujitetea kabla ya hakimu huyo kutoa hukumu, mshtakiwa huyo aliieleza mahakama hiyo kwamba hahusiki na vitu hivyo na kuitaka mahakama imwachie huru kwa kuwa kosa lililoletwa mbele ya mahakama hahusiki nalo huku akilitaka Jeshi la Polisi kumtafuta tena mmiliki halali wa viungo hivyo.
Mshtakiwa huyo, aliendelea kudai mahakamani hapo kwamba, siku ya tukio hilo hakuwepo nyumbani kwake
alikuwa shambani akilima kama ilivyo kawaida yake, lakini alishangaa aliporudi nyumbani akiwa na jembe lake begani, akawakuta polisi wamejaa nyumbani kwake na wakamkamata.

No comments:

Post a Comment