02 July 2013

VIJANA WASHAURIWA MBINU ZA KUJIAJIRI


 Na Darlin Said

VIJANA wameshauriwa kutotegemea ajira za kuajiriwa badala yake wajiajiri wenyewe kwa kujiunga katika vikundi vinavyotoa mikopo ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Thomas Tebaliwe wakati akisoma risala kwa wahitimu wa Chuo cha Eagle Wings.
Tebaliswe alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa.
Pia aliwashauri wahitimu hao kutumia elimu yao katika kujiajiri kwa kuchangamkia fursa zilizopo ili kuepuka kuwa tegemezi.
"Msitegemee kuajiriwa kwani kitendo cha kujiajiri wenyewe kwa kujiunga katika vikundi vinavyotoa mikopo ni njia mojawapo ya kujikwamua kiuchumi," alisema.
Katika mahafali hayo ambayo ni ya kwanza tangu kuanzishwa kwa chuo hicho zaidi ya wanafunzi 30 walihitimu mafunzo yao katika kozi mbalimbali.

No comments:

Post a Comment