Na
Suleiman Abeid, Kishapu
MB U N G E w a J i m b o la Kishapu mkoa
wa Shinyanga, Suleiman Nc h amb i ame z i n d u a rasmi mpango wa
kuvikopesha pikikipiki kwa masharti nafuu ya bila riba yoyote vikundi vya
vijana wanaoendesha pikipiki za bodaboda wilayani humo.Akizungumza kwenye sherehe fupi ya
mapokezi ya pikipiki 20 za awali zilizogharimu kiasi cha sh.milioni 42
zilizofanyika juzi katika kata za Bubiki, SekeBugolo, Mwigumbi na Songwa,
Nchambi alisema mpango huo ni moja ya ahadi zake alizozitoa wakati wa kipindi
cha kampeni mwaka 2010
. Kila kijana atakayekopeshwa pikipiki
kupitia kikundi chake atapaswa kulipia asilimia 30 ya bei halisi ya pikipiki
ambapo kiasi kinachosalia kitalipwa kwa utaratibu utakaopangwa na vijana
wenyewe na baada ya kukamilisha marejesho pikipiki itamilikiwa na kijana
aliyekopeshwa.Nchambi alisema mbali ya kutekeleza
ahadi hiyo lakini pia anaamini kupitia pikipiki hizo vijana wengi wilayani
Kishapu wataweza kujiajiri wenyewe na zitawakomboa kutoka katika dimbwi la
umaskini ambapo mpango huo utakuwa endelevu mpaka atakapokoma kuwa mbunge wa
jimbo hilo.
"Ni imani yangu kwamba kupitia mpango huu
vijana wengi katika jimbo letu wataweza kujiajiri wenyewe na hili ni zoezi la
kudumu, leo hii tumepokea pikipiki 20, lakini kutokana na asilimia 30
itakayolipwa na wakopaji wa mwanzo, tutaongeza pikipiki sita na hizo sita
zitaleta pikipiki nyingine mbili," alisema
No comments:
Post a Comment