02 July 2013

UVCCM WAKIKOSOA CHAMA CHAO CCM



 Na Andrew Ignas


UO N G O Z I w a U m o j a wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Kata ya Tandika wilayani Temeke, Dar es Salaam umesema umechoshwa na mwenendo wa chama kutowapa kipaumbele baada ya uchaguzi.
Hayo yalisemwa juzi na Kamanda wa vijana wa UVCCM katika kata hiyo ambaye pia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Kisarawe, Zena Mgaya wakati wa kufunga Baraza Maalumu la Vijana Kata ya Tandika.
Baraza ambalo liliambatana uzinduzi wa mashina ya UVCCM Kilimani na Sateta ambayo yalizinduliwa na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam, Omari Matulanga.
"Hili lipo wazi, sasa nasema ni mwisho kama wanachukulia sisi ni kama watu tunawanadia sera zao ili wachukue nchi basi imefikia mwisho, tumechoshwa," alisema Zena Mgaya. 

No comments:

Post a Comment