Na Grace Ndossa
CHAMA cha Wafanyakazi wa Viwanda,
Biashara Taasisi za fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) kimekosoa mfumo wa elimu
nchini kwa kile kilichoelezwa kuwa haukidhi matakwa ya soko la ajira duniani
.Pia kimesema
kuwa mfumo wa elimu uliopo hauzalishi wataalamu wa kutosha wa fani mbalimbali
wanaoweza kufanya kazi kwa weledi katika sekta mbalimbali ndiyo maana kwenye
sekta binafsi nchini, kazi nyingi za juu zinafanywa na wageni huku Watanzania
wakiendelea kubaki katika ajira zisizo na uhakika.
Hayo
yalibainishwa mwishoni mwa wiki na Katibu mKuu wa TUICO, Boniface Mkakatisi,
alipokuwa akizindua baraza la Katiba la chama hicho. Alisema asilimia kubwa ya
kazi zenye kuhitaji ujuzi na sifa za juu zinaendelea kufanywa na wageni huku
Watanzania walio wengi wakibaki hawana kazi.
"Pamoja na mapitio ya rasimu ya
katiba, nchi yetu haina budi kufanya mabadiliko makubwa katika sekta ya ajira ,
lazima Serikali ikubali mfumo wa elimu uliopo haukidhi matakwa ya soko la ajira
duniani," alisema Mkakatisi.
Alisema rasimu ya katiba mpya inatakiwa
kuhakikisha kuwa ajira za kutosha zinatengenezwa, mazingira ya kazi
yanaboreshwa na wafanyakazi wanalipwa ujira na mishahara yenye staha kwa ajili
ya kuwawezesha kumudu gharama za maisha pamoja na kuwapa morali wa kufanya kazi.
Hata hivyo alisema kuwa pamoja na ugumu
wa mazingira ya kazi, mishahara duni na hali ngumu ya maisha bado kipato cha
mfanyakazi kinaendelea kupungua kutokana na kiwango kikubwa cha kodi ambayo ni
chanzo kimojawapo cha Serikali katika mapato.
Mkakatisi alisema vyama vya wafanyakazi vimewahi
kutoa maoni mwaka jana na walipendekeza kiwango cha malipo ya kodi kipungue
kutoka asilimia 14 hadi 9.
No comments:
Post a Comment