02 July 2013

NEEC LAFADHILI WATANO KUSHIRIKI MAONESHO


BARAZA la Taifa la uwezeshaji Wa n a n c h i Ki u c h umi (NEEC),limewafadhili zaidi ya wafanyabiashara wadogo wadogo 50 kushiriki katika maonyesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, anaripoti Rehema Maigala.

Afisa Mwandamizi wa Uwezeshaji wa NEEC, Edward Kessy alisema jana kuwa mwaka huu wamefadhili makundi ya seremala, ushonaji, usindikaji vyakula, ufumaji na wale wanaoongeza thamani bidhaa zao lengo ikiwa ni kuwawezesha kupata masoko.
Al i s ema mi o n g o n i mwa wajasiriamali hao wako wanaotoka mikoa yaa Mbeya, Mtwara na Kibaha wakiwa na bidhaa za aina mbalimbali zinazotengenezwa na kampuni za kizalendo.

"Hapa wanaonyesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza na teknolojia wanazotumia katika kutengeneza, NEEC inaona hii ni fursa kwao kupata mbinu za kutafuta masoko na namna ya kuboresha bidhaa zao ili wakamate masomo ya kimataifa," alisema.
Alisema hata ushindi walioupata mwaka jana ulitokana na jitihada kubwa walizofanya kuwawezesha wajasiriamali wa kada mbalimbali kushiriki maonyesho na katika kuanzisha miradi mbalimbali.
Alisema huu ni mwaka wa tatu mfululizo wanawawezesha wajasiriAmali kushiriki maonyesho hayo kwa lengo la kuwafungulia masomo ya ndani na nje ya nchi.
"Wajasiriamali kuja hapa wenyewe inakuwa ngumu kutokana na gharama sasa, kila mwaka NEEC tunatarajia kuwezesha wajasiriamali zaidi kuja hapa kwa ajili ya kuonyesha bidhaa zao itawapa fursa nzuri kibiashara," alisema.

No comments:

Post a Comment