KAMPUNI ya TATA African Ho l d i n g s ( Ta n z a n i a ) L t d inayojishughulisha na uuzaji wa magari imekabidhi magazi zaidi ya 30 kwa Kampuni ya Usafirishaji jijini Dar es Salaam (UDA) kwa lengo la kupunguza tatizo la usafiri, anaripoti Benard Bugoma
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa UDA Bw. Hamidy alitoa wito kwa wananchi wa jiji hilo kuyajali magari hayo na kuuona mradi huo kama ni wao kwani kampuni hiyo haipo kibiashara bali kuwasaidia wakazi hao."Naomba kila mmoja awe mlinzi awapo kwenye basi, msisite kumbainisha mtu yeyote utakayemuona kwa makusudi anafanya uharibifu wa namna yoyote ile ndani ya basi," alisema Bw. Hamidy.
No comments:
Post a Comment