29 July 2013

TANESCO KUKABILI MGAWO VIWANDANI



 David John na Penina Malundo
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekutana na shirikisho la Chama cha Wamiliki wa Viwanda nchini (CTI) kwa lengo la kuzungumzia mikakati kabambe ya kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara hasa katika viwanda.Mkutano huo uliohudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felshers Mramba Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika ofisi za shirika hilo ambapo aliwaambia wanachama hao kuwa Shirika la Umeme limekuwa likipambana na kuimarisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika nchini.

Alisema Shirika linatambua fika matatizo yanayojitokeza katika kupata umeme wa uhakika nchini hasa katika Mkoa wa Dar es Salaam hivyo ili kuhakikisha tatizo hilo linapata ufumbuzi wa kuongeza upatikanaji wa vituo vitano vitakavyo fanya kazi ya kusambaza umeme katika Mkoa wa Dar es Salaam."Shirika linatambua fika changamoto kubwa iliyopo kuhusu umeme ndiyo maana Serikali kupitia TANESCO wameweza kuingia mikataba mingi ya kuanzisha vituo mbalimbali vya kuzalisha umeme ili kuwezesha huduma hiyo kupatika kwa uhakika," alisema.
Alisema tayari mpaka sasa vituo zaidi ya vitano vipo katika ujenzi wa kuwezesha kusambaza na kuponza umeme katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam,vituo hivyo ni pamoja na Mbagala,Gongo la mboto, Kurasini, Kinyerezi, pamoja na katika ya jiji hivyo kuna uhakika baada ya ujenzi huo tatizo la umeme litakuwa limepatiwa ufumbuzi.
Aliongeza kuwa mbali na vituo hivyo ambavyo vipo Dar es Salaam lakini Serikali imeweza kuingia mikataba mikubwa ya upatikanaji wa huduma ya umeme Tanzania ,ambapo pia huduma hiyo itaunganishwa hata kwa baadhi ya nchi jirani kama Nairobi, Ethiopia Zambia na itapita katika Mikoa wa Mtwara.Aliitaja mikoa mingine ni pamoja Singida,Mbeya, Shinyanga, Somanga , Arusha na Mikoa ya North West Grid ambayo ni Geita, Kahama, Nyakanyanzi na Kigoma.
Pia aliwaambia wadau hao kuwa Shirika linatambua hasara mbalimbali inayojitokeza pindi matatizo ya umeme yanapotokea, lakini aliwahakikishia kuwa ongezeko la vituo hivyo hasa katika jiji la Dar es Salaam litawezesha kuimarisha upatikana wa umeme katika viwanda na sehemu nyinginezo.
"Tunajua kuwa Shirika la TANESCO kwa asilimia 60 linategemea kuongeza pato lake kupitia viwanda hivyo nasi hatuwezi kuwaangusha kwani tunatambua kuwa nyie ni wateja wetu wa kubwa.na ili kuhakikisha hampati hasara ya kuharibika kwa vifaa vyenu pindi matatizo ya umeme yanapojitokeza,tumejipanga kuleta hu dumayamr adiwakud hibiti nakutoa taa r ifakwa wa katikamakunakuwanatatizololote la umeme."alis ema Mramb a.
Katika hatua nyingine Shirika hiloli mes ema limeku tananawada uwaKampuni zasimu za mkononi ilik ujadilin amnashi rika linavyoweza kutumi ahudu mazaombalimbali kwaku toataarifazamabadili yaumem ekwa wanan chi wake ,ambapom udaw owote wateja wotewataanza kupat ataarifakupitiasimu zao za mkononi.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa CTI, Felix Mosha alisema wanachama wake wanaona mabadiliko makubwa ya kuridhisha shirika hilo ukilinganisha miaka michache ya nyuma, hivyo ni matumaini kuwa uboreshwaji huo uwe na ubora na uhakika zaidi.
"Tunachoweza kusema ni kwamba TANESCO imekuwa ni mpya na endapo mtakapokuwa mnakwamishwa na fedha basi msisite kutuambia mapema ili nasi tuweze kuona namna ya kuweza kulisaidia shirika,"alisema Mosha.

No comments:

Post a Comment