Na Elizabeth Joseph, Dodoma
MA A D H IMI S H O y a
kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa Mkoa wa Dodoma
yameingia doa baada ya kukosa msisimko wa kutosha kutokana na maandalizi duni. Hali hiyo ilijitokeza siku ya jana katika maadhimisho hayo ambapo
mwitikio wa wananchi haukuwa wa kutosha hali iliyosababisha baadhi ya watu
kuhoji na wengine kulalamika kutokuwa na taarifa mapema.
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Mkoa wa Dodoma, Job Lusinde akielezea siku hiyo
alisema kuwa kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni kumekuwa na msisimko mdogo
tofauti na zamani na kuongeza kuwa juhudi inahitajika kufanywa ili kuwaenzi
vyema mashujaa hao.
Aidha Lusinde alikemea na kulaani kitendo cha baadhi ya wanasiasa
wanaochochea umwagaji damu nchini na kusema wanapaswa kuacha mara moja kwani
kwa kufanya hivyo amani na umoja wa nchi yetu vita itatoweka.
Naye Meja Jenerali Mstaafu Johnick Risasi ambaye pia alishiriki
katika vita hiyo ya Kagera alisema kuwa ameangushwa na msisimko mdogo wa
maandalizi hayo kwakuwa Manispaa ya Dodoma
pamoja na wananchi wake wanapaswa kuenzi siku hiyo.
Risasi aliongeza kuwa Serikali pia inatakiwa kuandaa utaratibu wa
kutenga eneo maalum ikiwemo makaburi ya mashujaa hao waliotangulia kwa
kuyahifadhi vizuri pamoja na kuwajali watu waliopata ulemavu katika vita hiyo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Nchimbi
aliwataka wananchi kuyaenzi maadhimisho hayo kama darasa la kujifunzia na
kujiuliza wanawaheshimu vipi mashujaa hao waliotangulia pamoja na kuwataka
kutii sheria bila shuruti kwa kuwaenzi bila kumwaga damu kwa kudumisha uhuru,
umoja, upendo na amani ambavyo vililetwa na mashujaa hao.
No comments:
Post a Comment