Na Lilian Justice,
Morogoro
.SERIKALI mkoani M o r o g o r o
imeziangukia Asasi za kiraia mkoani humo ikizitaka kuelekeza nguvu zake katika
kutekeleza vipaumbele vitano vya kitaifa na vilivyoelekezwa na Serikali ili
kuinua mkoa na taifa .Hayo yamefahamika mwishoni mwa wiki
kwenye mkutano wa Katibu tawala mkoa huo, Elia Ntandu alipokutana na baadhi ya
viongozi wa asasi hizo mkoani humo na kuwaeleza dhamira yake ikiwemo kutambuana
kwa kupeana taarifa fupi yenye historia, kazi zilizofanywa na asasi husika na
mipango yake ya baadae.
"Mbali na kufahamiana nimewaita
niwape dira na vipaumbele vya Serikali katika kuinua uchumi na kuukabili
umaskini, sasa vipaumbele vya Taifa ni vitano ikiwemo kukuza sekta ya kilimo,
maji, nishari, elimu na mawasiliano na kimsingi Morogoro imepewa dhamana ya
kuzalisha mchele na sukari katika kiwango cha kutosheleza mahitaji ya
nchi," alisema Ntandu.Akifafanua juu ya azma yake Katibu
Tawala huyo wa mkoa alisema angependa kuifahamu kila asasi inachokifanya kwa
jamii ili wapeane majukumu na kujiwekewa utaratibu utakao wezesha dira ya
serikali kutekelezeka kwa wakati na kwa faida ya watu wote kama ilivyo kwenye
dhamira za asasi hizo na serikali kuu.
"Labda kwa namna moja au nyingine
niseme mpango wa ushirikiano kati ya sekta ya umma, yaani serikali, na sekta
binafsi imeonyesha kuleta mafanikio makubwa ya maendeleo kwa jamii na kupitia
mpango huu mimi nimeamua kuanza na ninyi ili tujipange twende vipi..., sijui
naeleweka jamni," alifafanua zaidi.
Hata hivyo alipowataka kutoa changamoto
na nini kifanyike baadhi ya wajumbe wa mkutano huo waliirushia lawama Serikali
katika ngazi zote kutotoa ushirikiano kwa asasi hizo na kuanzisha uhasama kati
yake na asasi hizo kwa kilichodaiwa kuhisiwa ni vibaraka wa vyama vya siasa.
"Kuna changamoto nyingi lakini leo
tukutajie chache mfano hakuna uhusiano wa karibu kati ya watumishi wa umma na
sekta hii binafsi, tunapata vitisho hata vya kuuawa, taarifa zetu zinafichwa
baada ya tafiti na wengine tunatajwa kuwa wafuasi wa vyama vya siasa..., hii ni
hatari kuu," alisema Charles Mengele.
Aidha kwa upande wake Katibu wa umoja
wa asasi hizo mkoa, Iddi Mdanku alisema mbali na changamoto zinazozikabili
asasi hizo zimewezesha kukabili changamoto zilizo katika jamii na kuharakisha
maendeleo katika baadhi ya sekta na jamii.
Mdanku alisema kutokana na mpishano wa
kimawazo wamejikuta wakifanya kazi kwa kupishana na kusababisha kuonekana kama
za kichonganishi kutokana na watendaji wengi serikalini kufanya kazi kwa
mazoea.
Hata
hivyo katika mkutano huo walikubaliana kuunda timu itakayowakutanisha mara kwa
mara kuboresha utumishi, watumishi wa umma uwajibikaji kwa mujibu wa sheri,
kuwekwa ukurasa wa asasi kwenye tovuti ya mkoa, asasi wilayani kuandaa
wawakilishi na agizo la Rais wazee kufutiwa kodi na huduma bure litekelezwe
No comments:
Post a Comment