Na Israel Mwaisaka, Kyela
WATU watatu akiwemo wakala wa pembejeo
za kilimo katika Kata ya Ngonga wilayani Kyela, Geofrey Wanyato wamefikishwa
katika Mahakama ya Wilaya Kyela na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) wakikabiliwa na makosa 16 ya rushwa
A k i w a s ome a ma
s h t a k a watuhumiwa hao mbele ya Hakimu wa Mahakama hiyo ya Wilaya, Joseph
Luambano na Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Joseph Mlebya alisema kuwa
mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa ni wakala na wenzie wawili ambao ni Steven
Mwaipaja ambaye alikuwa ni ofisa mtendaji wa kijiji cha Ngonga na Alex
Mbanganile mwenyekiti wa kamati ya vocha ya kijiji wote walikula njama na
kuiibia halmashauri ya wilaya sh milioni 4.6
Alisema kuwa
mtuhumiwa wa kwanza ambaye alikuwa ni wakala wa pembejeo katika mwaka wa
2011-12 alighushi nyaraka ambazo ni vocha na fomu za wakulima na kumwibia
mwajiri wake ambaye ni Halmashauri ya Wilaya ya Kyela na kufanikiwa kumwibia sh
milioni 4.6 na kuiingizia hasara kubwa halmashauri ya wilaya.
Ambapo ofisa mtendaji
wa kijiji na mwenyekiti wa kamati ya vocha ya wilaya wao walimsaidia mtuhumiwa
kutenda kosa hilo na kumwezesha kujipatia fedha hizo hivyo wote kwa pamoja ni
wakosaji na wametenda kosa la jinai
Mwendesha mashtaka
huyo wa TAKUKURU a l i i e l e z a mahakama hiyo kuwa makosa mengi yanafanana
ila yamekuwa yakijirudia kwa tarehe tofauti hadi kufikia makosa 16 ambayo yameisababishia
halmashauri ya wilaya hasara kubwa lakini pia kuwanyima haki yao wakazi wa
Ngonga ambao ni wakulima kushindwa kupata pembejeo za kilimo
Washtakiwa wote kwa pamoja wamekana mashtaka yao
yote na wapo nje kwa dhamana hadi hapo kesi yao itakapotajwa Agosti 22 mwaka huu
No comments:
Post a Comment