Na Kassim Mahege
UMOJA wa Vyama vya Demokrasia
Duniani(IYDU)umeungana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kuitaka
Serikali kuunda tume huru ili kuchunguza watu wanaohusika na machafuko nchini.Imedaiwa iwapo
Serikali itashindwa kufanya hivyo itashtakiwa kwa nchi wanachama 80 wa umoja
huo wanaoamini demokrasia ya kweli ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa.
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa umoja huo, Aris Kalafatis
alisema wao wanaunga mkono suala la kuundwa tume huru ikiwa ni pamoja na
kufanyika uchunguzi wa wazi ili kuweza kuwapata wahalifu ili kulinda heshima ya
nchi.
"Umoja
wetu utahakikisha kuwa ripoti ya machafuko tuliyopewa tunaipeleka kwa wanachama
wenzetu wote duniani na kuwaita ili waweze kuiambia Serikali ya Tanzania
iheshimu demokrasia," alisema Kalafatis.Mwenyekiti huyo
alisema, umoja huo unaamini kuwa demokrasia ya kweli huishi na watu pasipo
kutumia nguvu ikiwa ni pamoja na kutoa uhuru wa kuchagua viongozi wanaokubalika
na wananchi bila vitisho.
Alisema, ripoti
waliyopewa na Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA)
inaonyesha kuwa Tanzania kuna ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu, mauaji kwa
wananchi wasiokuwa na hatia.Sambamba na
vitendo vya utekaji nyara kwa watu wasiokuwa na hatia akiwemo Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Madaktari Tanzania, Dkt. Stephen Ulimboka na wengine.
Alisema, mwaka
2012 umoja huo ulilaani mauaji ya mwandishi wa habari aliyekuwa akiripoti
CHADEMA, Daudi Mwangosi kupitia polisi na kuongeza kuwa bado matukio hayo
yanatia wasiwasi mkubwa kwa umoja huo."Umoja
wetu pia umepewa idadi ya watu wasiokuwa na hatia waliotekwa ikiwa ni pamoja na
mlipuko wa bomu kule Arusha na kusababisha mauaji ya watu watatu...lakini
Serikali imekaa kimya," alisema Mwenyekiti huyo.
Kwa upande wake
Katibu Mkuu wa BAVICHA, Deo Munishi alisema ugeni huo umekuja hapa nchini Julai
25, mwaka huu ambapo wamepata nafasi ya kutembelea maeneo mbalimbali ili
kujionea hali halisi ya nchi.
Alisema, umoja huo una vituo vyake
zaidi ya 120 na washiriki kutoka nchi zaidi ya 80 duniani ambapo umejikita
katika kutetea demokrasia ya kweli, haki za binadamu, siasa safi, uchumi na
kupigania maendeleo.
Hakuna ukweli wowote wa hiyo Taarifa ya IYDU inaelemea zaidi BAVICHA kupata ukweli fuatilia uione You Tube wenzao wa IYF wanavoimba na kuipongeza Tanzania 'Nakupenda Tanzania http://t.co/Jzn09Awl4b
ReplyDeleteUnapoteza muda kupigia upatu chadema. Tanzania ingelalamikiwa ingeweza kuleta vigogo wote wa dunia na kuisifia. Mnatengeneza mazingira ya serikali kutumia nguvu zaidi. Manaopotosha umma na mmefaulu kupandikiza chuki kwa wanchi. Sijui hicho chama kikiingia madarakani kitawalipa nini wananchi wanaodanganywa kila kukicha.
ReplyDelete