LONDON, Uingereza
SALAMU z a p o n g e z i zimekuwa
zikimiminika kutoka pande zote za dunia kusherehekea kuzaliwa kwa mtoto wa
kiume wa Prince William na mkewe Kate. Mtoto huyo anakuwa wa tatu katika orodha
ya kurithi kiti cha ufalme.Maelfu ya watu
waliokuwa wakiwatakia mema walimiminika katika jumba la kifalme la Buckingham
baada ya taarifa hizo kuvuja.
Uzazi huo wa
kifalme baadaye unatarajiwa kupewa heshima kwa milio ya bunduki na kupigwa
kengele za Westminster Abbey. Prince William alikuwepo katika
Hospitali ya Mt. Mary, Magharibi mwa London, akisubiri na alishinda usiku na
Catherine pamoja na mtoto huyo baada ya kuzaliwa. Msemaji wa Jumba la Kensington alisema
ilikuwa "mapema mno" kusema kama wangeruhusiwa kutoka hospitali jana.
Wanandoa hao walitarajiwa kuongea na
timu yao ya madaktari kabla ya uamuzi kufanyika.Kwa mujibu wa BBC, uwezekano haukuwa
mkubwa kwa Malkia kumtembelea kitukuu chake hospitali, lakini iliongeza kusema;
"bila shaka anaweza kumtembelea akiwa binafsi atakapoondoka hospitali".
Baada ya taarifa ya kuwasili kwa
mtoto huyo kutangazwa na jumba la kifalme la Kensington, umati mkubwa wa watu
pamoja na waandishi wa habari ulishangilia nje ya hospitali.
No comments:
Post a Comment