Mwajuma
Juma, Zanzibar
na Cresensia Kapinga, Songea
ASKARI saba wa Jeshi la Ulinzi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
waliouawa katika shambulio la kushtukiza mjini Darfur, nchini Sudan wamezikwa
jana katika mikoa mbalimbali walikokuwa wakitoka.
Askari hao
walizikwa kwa heshima zote za kijeshi kwenye mazishi yaliyoongozwa na viongozi
mbalimbali wa kitaifa na kimikoa. Visiwani
Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, aliungana na viongozi mbalimbali wakiwemo
wa vikosi vya ulizi na usalama wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania,
wafiwa na wananchi katika mazishi hayo. Askari kutoka Zanzibar waliozikwa ni Shaibu Othman na Mohamed Juma Ally.Dkt. Shein akiwa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Shariff Hamad, walishiriki katika dua ya hitma iliyosomwa kwa ajili ya askari hao na kuwasalia katika Msikiti wa Noor Mohammad (S.A.W), Mombasa kwa Mchina, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja. Wananchi,wafiwa na viongozi mbalimbali wa vyama na serikali walihudhuria hitma hiyo. Awali Dk. Shein aliweka saini kwenye vitabu vya maombolezi kwa ajili ya marehemu hao.Baada ya kumaliza dua na swala kwa ajili ya askari hao, Dkt. Shein, aliongozana na viongozi wengine na wananchi kwenda kwenye Makaburi ya Mwanakwerekwe kwa ajili ya mazishi. Katika makaburi ya Mwanakwerekwe mamia ya wananchi walijitokeza kwa wingi kwa ajili ya kuwaaga marehemu hao ambapo wote wamezikwa katika eneo hilo maarufu la Makaruni liliopo Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.Makaburi ya askari hao yalichimbwa jirani. Miili ya askari hao ilizikwa kwa taratibu zote za kijeshi na baadaye kufuatiwa taratibu za kidini.
Baada ya mazishi kumalizika zilizomwa
salamu za Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete. Katika salama zake Rais Kikwete,
alimuomba Mungu aziweke roho za marehemu hao mahali pema peponi.
Rais Kikwete, alisema msiba huo ni wa
Taifa zima na si kwa upande wa Tanzania pekee, bali ni Afrika na dunia nzima
kwa ujumla.Nao wanafamilia na wazazi wa marehemu
hao, walitoa shukrani zao za dhati kwa Serikali zote mbili kwa juhudi kubwa
zilizochukuliwa kuhakikisha marehemu hao wanafika kwenye familia zao na kuzikwa
kwa taratibu zote.
Mjini Songea simanzi, vilio na majonzi
vilitawala wakati wa mazishi ya askari wa JWTZ, Rodney Ndunguru, wa kikosi cha
makomando cha 92 KJ Ngerengere mkoani Morogoro.Mazishi hayo yalihudhuriwa na mamia ya
wakazi wa Mkoa wa Ruvuma wakiwemo askari.
Mazishi hayo yalifanyika jana kwenye makaburi ya Mjimwema Manispaa ya Songea.
Katika mazishi hayo yaliyongozwa na
Paroko wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Songea Parokia ya Mjimwema, Padre Noel
Duwe. Katika mahubiri yake alitaka Watanzania kutochezea amani na kwamba
utulivu walionao Watanzania unahitajika kulindwa kwa namna ya aina yoyote na si
vinginevyo.
Padre Due alisema kwa wale wote
wanaotaka kuchezea amani na utulivu tulionao wanapaswa kukemewa kwa nguvu zote
kwa kuwa Watanzania hawakuzoea vurugu.Kwa upande wake msemaji wa familia ya
marehemu, Ndunguru alisema familia imepata pengo kubwa kwa kuondokewa na kijana
wao na ameiomba serikali kuangalia uwezekano wa kuisaidia.
Alisema kuwa Rodney amefariki akiwa na
miaka 28 ambapo kimsingi kifo chake kimeacha pengo kubwa kwa famila kwani
katika uhai wake ilikuwa faraja kwa ndugu.
Wakati huo huo, habari
ambazo gazeti hili limepata wakati likienda mtamboni zinaeleza kuwa wanajeshi
wa JWTZ waliokuwa wakitoka kwenye mazishi ya wenzao waliouawa mjini Darfur
wamepata ajali mjini Zanzibar,
eneo la Mwanakwerekwe, umbali wa mita 300 kutoka kwenye makaburi.
No comments:
Post a Comment