24 July 2013

KIWANDA CHA BUNDUKI CHAGUNDULIKA DAR


  • MMLIKI WAKE ADAIWA KUKODISHA BUNDUKI KWA MAJAMBAZI
  • ANAYETAPELI KWA JINA LA MCHUNGAJI RWAKATARE MBARONI
 Leah Daud na Josephine Burton
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limekamata kiwanda cha kutengeneza kienyeji bunduki za aina mbalimbali maeneo ya Kawe, wilayani Kinondoni.Kiwanda hicho kinadaiwa kumilikiwa na mkazi mmoja aliyetajwa kwa jina cha Charles Masunzu (30). Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi, Kanda Maalum Dar es Salaam, Ally Mlege, alisema baada ya kukamatwa kwa mmiliki huyo, aliwataja majambazi ambao amekuwa akiwakodisha silaha zake kwa ajili ya kwenda kufanya uhalifu.

Walitaja watu hao kuwa ni Matola Rashid (27), Omary Hassan (43), Martha Mhagama(32) na Mwasiti Maulid (22).Alisema watuhumiwa hao walikamatwa na bunduki aina ya SMG iliyosajiliwa kwa namba 02704 ikiwa na risasi 20 ambapo ilikuwa imekatwa kitako. Alisema majambazi hao baada ya kuhojiwa walikiri kujihusisha na matukio ya uporaji sehemu mbalimbali za jijini Dar es Salaam kwa kutumia silaha. Alisema kwamba majambazi hao walikiri kumpora silaha Polisi Wilayani Rufiji akiwa anasindikiza magari kutoka Ikwiriri Mkoa wa Pwani mwaka 2007.
Alisema mtuhumiwa anayedaiwa kumiliki kiwanda cha silaha alipopekuliwa alikutwa akimili bunduki mbalimbali, ikiwemo SMG namba 2539 Double Bore. Rifle tatu, Fiffe Mark tatu, Rifle Mark 3 Pistol KJW Works, mitutu mitano iliyotengenezwa kienyeji, pingu, risasi 36, maganda 17 ya risasi, mkebe wa gololi za silaha aina ya SMG na mifuko ya kuhifadhia silaha.Pia alisema mtu huyo alikamatwa pia na vifaa vingine vikiwemo vya kutengenezea silaha za kienyeji, mikasi minne aina tofauti na mipini mitatu ya silaha aina ya Rifle. Pia mtu huyo pia alikamatwa na vifaa vingine vya aina mbambali.
Katika tukio lingine, Jeshi la Polisi limefanikiwa kumkamata mtu mmoja, Mfaume Omary maarufu kwa jina la Mau (29) anayetumia majina ya viongozi wa Serikali, dini na watu maarufu na kujipatia fedha kwa kuvaa uhusika wa mtu husika.
Alisema kwa hivi karibuni wamekuwa wakifuatilia nyendo zake baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mchungaji Getrude Rwakatare, kuwa jina lake linatumiwa vibaya na watu ili kujipatia fedha.
Mlege alisema jeshi la Polisi wa l i f a n i k iwa k umk ama t a mtuhumiwa huyo akiwa anamiliki simu namba 0659 736454 ikiwa imesajiliwa kwa jina la Mfaume Said Omary na 0659 164744 ikiwa imesajiliwa kwa jina la Alex Mtenga.
Alisema baada ya mahojiano na mtuhumiwa alikiri kutapeli watu mbalimbali wakiwemo wachezaji maarufu wa timu za mpira hapa nchini kwa kuvaa uhusika wao.
Hata hivyo alisema mtuhumiwa huyo anaendelea kushikiliwa kwa mahojiano na atafikishwa Mahakamani baada ushahidi kukamilika.Wakati huo huo, Kamishna Mlege alisema Polisi wanamsaka mtu anayetuhumiwa kummwagia tindikali Mkurugenzi wa Home Shopping Center, Said Mohamed Saad.



No comments:

Post a Comment