Na Mashaka Mhando, Korogwe
MBUNGE wa Jimbo l a K o r o
g w e , Stephen Ngonyani Profesa Majimarefu, amesema atakuwa tayari kujiuzulu
nafasi yake ya ubunge endapo atashindwa kutekeleza ahadi zake zilizomo kwenye
Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 hadi 2015. Akizungumza katika uwekaji wa
jiwe la msingi la Kituo cha Polisi cha Tarafa ya Magoma lililokuwa likiwekwa na
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni (Mstaafu) Chiku Gallawa, mbunge huyo alisema kuwa
atakuwa tayari kujiuzulu endapo hatatekeleza ahadi zake na kwamba, kazi
anazozifanya kila anapopata fursa za kutembelea jimbo hilo, amekuwa akitekeleza.
Mbunge huyo
alianza kuanisha kazi mbalimbali ambazo amezifanya katika tarafa hiyo, ikiwemo
kutoa bati 60 zenye thamani ya shilingi milioni 2.6 kwa ajili ya kuezekwa
kwenye soko lililopo katika Kijiji cha Magoma, kiasi cha shilingi milioni 1 kwa
ajili ya kusaidia shule ya Sekondari Magoma.
Alimwambia mkuu huyo wa mkoa hata
kukamilika kwa ujenzi wa jengo la mahakama ya mwanzo tarafa hiyo ya Magoma, ni
matokeo yake ya kuibana Serikali hasa Waziri wa Sheria kuhakikisha Tarafa hiyo
na Mkomazi zinajengewa mahakama ili kuondoa msongamano katika maeneo mengine.
Linginealilomwambia Mkuu huyo wa mkoa mbunge huyo, alisema kuwa ni suala la
umeme ambapo kwasasa wataalamu wa mpango wa uwekezaji umeme vijijini (REA),
wanatandaza nguzo katika vijiji mbalimbali vya tarafa hiyo kama
ambavyo amehakikishiwa na Waziri katika Bunge lililopita. " M h e s h i m
i w a k a z i tunafanya huku katika jimbo hili, nitakuwa tayari kujiuzulu
endapo ahadi nilizozitoa zitazitekeleza lakini naamini kwa ushirikiano na
wananchi hawa nitatekeleza ili mwaka 2015 chama chetu cha CCM tutembee kifua
mbele," alisema mbunge huyo. Mbunge huyo alisema atashauriana na watendaji
na viongozi wa Serikali ili bati 60 alizozitoa kwa ajili ya soko hilo, zibadilishwe matumizi na sasa bati hizo zipangwe
kuezekea kituo hicho cha polisi kisha halmashauri watakapokuwa tayari kulijenga
soko hilo,
atatoa bati nyingine
No comments:
Post a Comment