31 July 2013

TLSB YASAIDIA VITABU 3240



Na Mwandishi Wetu, Ngara
BODI ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB), imetoa vitabu 3,240 vyenye thamani ya sh.milioni 54.3 kwa ajili ya kuanzisha maktaba mbili za Wilaya ya Ngara, mkoani Kagera.Mkurugenzi Mkuu wa TLSB, Dkt. Alli Mcharazo, alisema hayo jana mara baada ya kuzinduliwa kwa Maktaba ya Wilaya ya Ngara na ile ya tarafa ya Rulenge
. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Dkt.Mcharazo alisema maktaba hizo zitakazokuwa zikiendeshwa na TLSB kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya zitasaidia kuleta maendeleo kwa jamii hiyo wakiwemo wanafunzi.Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, maktaba ya Ngara ilipewa vitabu 2,018 vyenye thamani ya Sh.milioni 36.9 na ile ya Rulenge ilipata vitabu 1,222 vyenye thamani ya sh.milioni 17.3.
  Mcharazo alisema pia bodi hiyo imetoa wakutubi wawili ambao watagawanywa katika maktaba hizo kwa ajili ya kuzisimamia."Tunafurahi kwamba wananchi wa Wilaya ya Ngara sasa wanaanza kupata huduma za maktaba ili kujifunza masuala mbalimbali yatakayowasaidia katika kuleta ma e n d e l e o y a o , " a l i s ema Mcharazo. Alisema hadi sasa bodi hiyo ina maktaba katika mikoa 21, wilaya 19 na tarafa 2 na kwamba juhudi zinafanyika kueneza huduma hiyo katika maeneo yaliyobaki hasa vijijini.
  Akizindua maktaba hizo, Mbunge wa Jimbo la Ngara, Deogratias Ntukamazina alisema wilaya hiyo imebahatika kuzindua maktaba mbili kwa wakati mmoja."Ni tukio tulilolisubiri kwa muda mrefu, jamii ya Ngara itapata maarifa kupitia maktaba hizo na hivyo kujiletea maendeleo yao," alisema Ntukamazina. Aliwataka wananchi wakiwemo wanafunzi kujitokeza kuzitumia maktaba hizo ili kujiongezea uelewa

No comments:

Post a Comment