Na Fatuma Rashid
KOCHA Mkuu wa Timu ya Taifa Stars, Kim
Poulsen amejitetea kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Uganda 'The Cranes' kuwa
kilitokana na wachezaji wake wengi kuwa katika mfungo wa Ramadhani.Katika mechi hiyo ya kuwania kucheza
fainali za Wachezaji Wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN), ilichezwa Uwanja wa
Mandela, ambapo katika mechi ya kwanza iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam Stars walifungwa bao 1-0.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Poulsen
alisema kuwa amehuzunika sana na kipigo hicho ingawa mfungo ulichangia lakini
hatakata tamaa.Alisema kuwa wachezaji walijipanga
walicheza vizuri, lakini ili mchezaji afanye vizuri anatakiwa apate chakula na
maji ya kutosha ila kutokana na mfungo ilichangia timu hiyo kutofanya vizuri.
"Kufunga pia kulichangia timu
kufungwa wachezaji walipungukiwa nguvu, pia kukosekana kwa wachezaji Mwinyi
Kazimoto na Shomari Kapombe kulileta pengo kubwa," alisema Kim.Aliongeza kwa sasa ana muda mrefu wa
kukiandaa kikosi chake vizuri hivyo Watanzania wasikate tamaa.Alisema kuwa kuna haja ya kuwaendeleza
wachezaji Vijana ili kuweza kuandaa wachezaji watakaoweza kuchezea timu ya
Taifa.
Pia kocha huyo aliahidi kuwa Watanzania
wataona mabadiliko makubwa hapo baadaye, kwani anaamini kutokana na makosa
madogo madogo aliyoyaona kwa baadhi ya wachezaji yanarekebishika.
"Umoja ni nguvu katika kila jambo
na tukishirikiana najua tutafanya vizuri,timu inapokuwa na mafanikio lazima
kuna kipindi inakwama na ndivyo ilivyotokea katika timu yangu lakini inabidi
tuangalie timu ilipotoka na inapoelekea," alisema.Poulsen
aliongeza kuwa hivi sasa timu hiyo inajiandaa na mechi yake dhidi ya Gambia
kukamilisha ratiba yao katika michuano ya kuwania kucheza Kombe la Dunia.
No comments:
Post a Comment