Na Thomas
Itembe,Tarime
MAMIA ya wananchi
Wilayani Tarime jana wamejitokeza kuhudhuria kumbukumbu ya kumuenzi aliyekuwa
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa
Wilaya Tarime, maheremu Chacha Wangwe
.Kumbukumbu ya
kumuenzi marehemu Wangwe ilianzishwa na aliyekuwa Diwani wa Kata ya Sabasaba,
John Heche, baada ya kufariki kwa ajali ya gari Julai, 2007 akiwa safarini
kutoka Dodoma kwenda jijini Dar-es Salaam.
Katika kumbukumbu
hiyo wa n a n c h i wa Ta r ime n a Tanzania kwa ujumla walitakiwa kumkumbuka
na kumuenzi kwa sababu alikuwa shujaa asiyeogopa na mtetezi wa wanyonge wakati
wa uhai wake.
Akizungumza wakati wa
kumbukumbu hiyo, Heche alisema, marehemu Wangwe hakukubaliana alikuwa mtetezi
wa akinamama wauza mboga na matunda, ambapo alipinga ushuru waliokuwa wakitozwa
hadi ukazuiwa na mahakama.
Heche alitumia nafasi hiyo kuwataka vijana wa CHADEMA kuacha malumbano
ndani ya chama badala yake wajenge nguvu ya pamoja kuimarisha chama kama hali
aliyokuwa nayo, marehemu Wangwe na kuwa wapinzani wao ni CCM si viongozi ndani
ya chama.
.
No comments:
Post a Comment