Na Habib Miradji
MKANDARASI anayejenga kipande cha
barabara ya Ndundu hadi Somanga , inayounganisha mikoa ya Pwani na Lindi,
kampuni ya MA Kharafi, amesema amejipanga kumaliza kazi za ujenzi wa mradi huo
kama alivyoelekeza Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli.Amesema
atafanya hivyo iwapo ataendelea kupata ushirikiano kutoka kwenye mamlaka
mbalimbali Serikalini zinazohusiana na utekelezaji wa mradi huo.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na mkandarasi huyo kwenye eneo la mradi hivi karibuni mara
baada ya ziara ya waziri Dkt.Magufuli, ilisema ufuatiliaji wa waziri huyo
umewapa matumaini mapya ya kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kabla ya Desemba
30,2013.Alisema hatua
hiyo itafikiwa iwapo waziri huyo atasaidia kuhimiza wadau wengine muhimu
kutekeleza majukumu yao kwa wakati yakiwemo malipo wanayodai.
T a a r i f a h i y o i n a t a j a
ucheleweshwaji wa malipo kuwa umesababisha mkandarasi kutumia zaidi ya sh.
bilioni 20 wakati wa kipindi cha kusimama mradi huo kwa kulipa mishahara
wafanyakazi wake na gharama za uendeshaji wakati wa kusubiri malipo.
“Ucheleweshwaji wa malipo unasababisha
hasara pia kwa Serikali kulipa fedha nyingi zaidi kuliko gharama za awali za
mradi huo,” ilieleza sehemu ya taarifa yake.
Taarifa hiyo ilibainisha kuwa moja ya
mikakati ya kujizatiti kukamilisha mradi huo ni kuongeza magari na mitambo
ambapo hivi karibuni wamenunua malori makubwa aina ya tipa 13 kwa ajili ya
kukamlisha kazi mapema.
Ilisisitiza kuwa malimbikizo ya malipo
wanayodai yakipatikana kwa wakati watanunulia mafuta ya kuendeshea mitambo hiyo
na kuifanyia matengenezo mitambo iliyoharibika.
“Mkandarasi si mfadhili wa mradi,
anapofanya kazi alipwe mara moja ili kazi nyingine ziendelee vinginevyo kazi
lazima zisimame na gharama kuongezeka,” ilieleza taarifa hiyo. Ilidaiwa kuwa
kutokana na usumbufu wanaoupata wangeweza kuvunja mkataba, lakini mahusiano
mazuri na serikali, ushirikiano, Dkt. Magufuli na Mkurugenzi Wakala wa Barabara
(TANROADS) Patrick Mfugale, ndio imemfanya kuendelea kuvumilia hadi
watakapomaliza mradi huo.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili
umebaini kuwa Wizara ya Fedha haijaidhinisha maombi ya mkandarasi huyo ya
misamaha ya kodi kwa ajili ya ununuzi wa mitambo uliofanywa na mkandarasi tangu
mwaka 2011 hadi 2013.Misamaha ambayo ipo kwenye mkataba ni
msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa ajili ya ununuzi wa mafuta ya
dizeli.
Mradi wa ujenzi wa sehemu ya barabara
hiyo ukikamilika utaunganisha Jiji la Dar es Salaam na mikoa ya kusini ambapo
ulisainiwa Juni 30, 2008 kati ya Serikali na kampuni ya MA Kharafi.Thamani ya mradi ilikuwa sh. bilioni 58.8. Awali
mradi ulipangwa kukamilika Januari 14, 2011 lakini kutokana na sababu
mbalimbali zilizo nje ya mkandarasi serikali ililazimika kumwongezea muda ili
kukamilisha kazi hiyo Desemba 30, 2013
No comments:
Post a Comment