03 July 2013

MAANDALIZI UCHAGUZI BFT YAKAMILIKA




Na Mosi Mrisho
MBIO za kuwania madaraka ndani ya Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), zimeanza na zinatarajiwa kuhitimishwa jijini Mwanza kesho ambapo uchaguzi huo utafanyika.
Akizunmgumza Dar es Salaam jana Afisa Michezo Msaidizi wa BFT Richard Mganga, alisema mpaka sasa wamejitokeza watu watano kuchukua fomu za kuwania uongozi ndani ya chama hicho.
Maganga alisema uchaguzi huo utafanyika baada ya viongozi wa sasa kumaliza muda wao wa uongozi kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.
Alisema wapo watu wengi wanaohitaji kuingia kwenye uongozi huo, lakini zipo sifa mbalimbali ambazo zinahitajika ili kuweza kushiriki uchaguzi huo.
Maganga aliongeza kuwa wadau kabla ya kufikiria kuingia BFT lazima wagombea wajichuje wenyewe, ambapo mgombea pamoja na elimu yake au kuwa na sifa nyengine anatakiwa kuwa na sifa za uongozi nauzoefu wakutosha.
Alisema mpaka sasa waliojitokeza kuchukua fomu za kuomba uongozi ni watano.

No comments:

Post a Comment