04 July 2013

MHANDISI MAHAKAMANI KWA KUGHUSHI RISITI


 Na Eliasa Ally, Iringa
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) , Mk o a wa Iringa imemfikisha mahakamani Mhandisi wa Idara ya Maji wilayani Ludewa, Mkoa wa Njombe, Athanasius Munge kwa kumdanganya mwajiri wake ambaye ni Mkurugenzi wa wilaya hiyo.
Udanganyifu huo unadaiwa unatokana na kumpelekea Mkurugenzi (hakutajwa jina) wa halmashauri hiyo risiti za malipo hewa yenye zaidi ya sh. milioni 21 kwa madai kuwa kuna wajumbe wa Idara ya Maji walikula na kunywa chai wakati wanatembelea miradi ya maji katika wilaya hiyo.



Wajumbe hao walidaiwa walijipatia chakula hicho katika mgahawa wa mfanyabiashara, Videa Kayombo mjini hapa ambaye anadaiwa kumpatia risiti feki ili waweze kujipatia fedha hizo.
A k i s oma ma s h t a k a y a watuhumiwa hao jana, Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Mkoa wa Iringa, PP Imani Mitume Mizizi kwa watuhumiwa hao wawili mbele ya Hakimu Hassan Juma wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa alisema watuhumiwa hao walifanya makosa ya kufoji risiti zao ili wajipatie malipo hayo.
Aidha, alidai katika makosa hayo Mhandisi Athanasius Munge alipatikana na makosa matano ambapo makosa manne yanamhusu na kosa la tano wameunganishwa na Videa Kayombo kwa kufoji risiti feki kwa nyakati tofauti za sh. milioni 21.
Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, alisema kosa la kwanza kati ya mwezi Oktoba 9 hadi 18 mwaka 2008 Mhandisi Munge alimpelekea risiti mwajiri wake kumtaka alipe kiasi cha sh. milioni 4.2 kwa madai kuwa wajumbe wa Idara ya Maji walifanya mkutano na kula chakula.
Sambamba na chai katika mgahawa wa Videa Kayombo; hivyo kukiuka Sheria ya Manunuzi namba 11 ya mwaka 2007.
Aidha, alisema kosa la pili, Mhandisi Munge akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Oktoba 7, 2008 alimpelekea mwajiri wake risiti namba 0004994 iliyotolewa katika Mgahawa wa Merelendi unaomilikiwa na Videa Kayombo akidai kulipwa sh. milioni 4.2 kwa madai kuwa wajumbe wa idara hiyo walikula chakula na chai wakati si kweli.
Mwendesha Mashtaka, Mzizi alisema kuwa kosa la tatu Oktoba 7, 2008 Mhandisi huyo alimpelekea pia mwajiri wake vocha ya malipo namba 21 kutoka katika Mgahawa wa Merelendi unaomilikiwa na Videa Kayombo kwa madai kuwa kamati ya wajumbe wa maji kutoka vijiji vya wilaya ya Ludewa walikusanyika na kula chakula pamoja na kunywa chai wakati si kweli na kumtaka Mkurugenzi kulipa malipo ya sh. milioni 4.2 kwa mwenye mgahawa huo.
Pia Mwendesha mashtaka huyo alisema, katika kosa la nne Mhandisi Munge alilifanya Oktoba 7, 2008 baada ya kumpelekea vocha feki ya malipo mwajiri wake namba 5/10 ambayo iliandikwa Oktoba 8, 2008 akidai kulipwa sh. milioni 4.2.
Alidai kuwa, wajumbe wa Mradi wa Maji wa NRWSSP walikula na kunywa chai katika Mgahawa wa Merelendi uliopo Ludewa ambao unamilikiwa na Videa Kayombo.
Mbali na hayo alidai kuwa, katika kosa la tano linawaunganisha washtakiwa wote wawili Mhandisi Munge na Videa Kayombo kwa kula njama za kuandaa hati feki za malipo ya sh. milioni 4.2 kwa nyakati tofauti kuanzia Oktoba 9 hadi 18, 2008 kwa kutaka kulipwa malipo ya fedha na Halmashauri ya Ludewa jumla ya sh. milioni 21 ambazo zilikuwa ni fedha hewa.
Katika kesi hiyo, watuhumiwa wote wawili walikana mashtaka ya kutohusika na hujuma hizo ambapo Mwendesha Mashtaka Mizizi alisema kuwa, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika ambapo alimwomba Hakimu tarehe ya kuanza kuisikiliza ikiwemo kuwaleta mashahidi.
Hakimu Hassan Juma ambaye alikuwa anasikiliza kesi hiyo aliahirisha kesi hiyo hadi Julai 15, mwaka huu ambapo watuhumiwa walirudishwa rumande baada ya kukosa wadhamini ambao wangekidhi masharti

No comments:

Post a Comment