Na Suleiman
Abeid, Shinyanga
CHAMA Ch a Demo k r a
s i a na Maendeleo (CHADEMA) kimewaomba Watanzania kuweka pembeni tofauti zao
za vyama vya siasa, dini na ukabila na waungane kujadili mustakabali wa nchi
yao, huku kikisisitiza suala la kuwajengea ukakamavu vijana wake wa Red Brigade.Kauli
hiyo ilitolewa juzi na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alipokuwa
akihutubia umati wa watu katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapa.Mbowe
alisema kuna kila sababu ya Watanzania kuungana pamoja na kukaa chini ili
kujadili mustakabali wa nchi inavyokwenda. Alisema kwa sasa kuna viashiria
vinavyoashiria amani na utulivu kupotea.
"Sisi
CHADEMA tunasema hali ya mambo yanavyokwenda hapa nchini siyo nzuri, kuna kila
sababu ya kukaa chini tuangalie tulikotoka, wapi tulipo na huko tunakokwenda,
na hii tusitangulize mbele itikadi za vyama vyetu vya siasa, udini au ukabila,
CHADEMA tunasema daima tutahubiri amani, nchi yetu sasa hivi inakabiliwa na
matatizo mengi, tutafute jinsi gani tutamrejea Mungu ili hali ya amani iweze
kuimarika, tusiangaliane kwa itikadi ya vyama vya siasa wala dini,"
alisema Mbowe.Akizungumzia
tukio la Arusha, mwenyekiti huyo alisema viongozi wote wa CHADEMA waliokuwa
katika mkutano ulioshambuliwa kwa kurushiwa bomu walinusurika kifo kutokana na
mipango ya Mungu ambapo alisema washambuliaji katika tukio hilo walitumia aina
nne tofauti za silaha.
"Tukio
la Arusha kusema kweli tulinusurika kwa mapenzi ya Mungu, maana tulishambuliwa
kwa silaha nne tofauti, kwanza kwa bomu liliua watoto na wanawake, kisha
zikafyatuliwa risasi za moto kwa kutumia SMG, lakini tukapigwa bastola, na
tulipojaribu kuokoa majeruhi tukapigwa mabomu ya machozi," alisema Mbowe.Aliongeza
kuwa; "Polisi tuliotegemea watulinde wote walikimbia kuondoka katika eneo
la tukio, hivyo tunaposema tutawajengea ukakamavu vijana wetu wa Red Brigade,
wenzetu CCM wasituelewe vibaya wala wasiogope, CHADEMA hatuhitaji jeshi la
kutumia silaha, tunataka ulinzi kwa viongozi wetu na kwenye shughuli zetu za
chama, kama wanavyofanya CCM wenyewe kupitia vikundi vya Green Guard."
Katika
kuthibitisha kuwa CCM inavyo vikundi vya Green Guard, Mbowe alionesha hadharani
kitabu cha Sera na misingi ya CCM ambacho ndani yake kinaelekeza masuala ya
kuwajengea uwezo vijana wake na waweze kupambana na vijana wa vyama vya
upinzani.Hata
hivyo alisema iwapo Watanzania watakataa chama hicho kisiwe na kikosi hicho wao
wako tayari kuachana na mpango huo na kama wataruhusiwa wataendelea kuwajengea
ukakamavu vijana wao kwa nia nzuri ya kuweka ulinzi katika shughuli zote za
CHADEMA.Aliwataka wapenzi na
wanachama wa CHADEMA kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni yao kwenye mabaraza ya katiba ambapo alisema
chama chake kinaunga mkono suala la uwepo wa Serikali Tatu.
No comments:
Post a Comment