Na Yusuph
Mussa, Korogwe
FITINA za kisiasa zimemfanya Mbunge wa
Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani (Profesa Majimarefu) kushindwa
kuwahutubia wapiga kura wake kwenye mkutano wa hadhara na kuanza kutokwa
machozi baada ya kubaini baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye
jimbo hilo
wamemchonganisha na Mwenyekiti wake Taifa, Rais Jakaya Kikwete.
Viongozi
hao wa chama chake walivitumia vyombo vya habari kufikisha ujumbe kwa Rais
Kikwete kwa kusema Mbunge huyo na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mrisho Gambo
wanawapendelea zaidi wakulima kuliko wafugaji, ndiyo maana hata baada ya tukio
la kuchomwa nyumba 16 za wafugaji wa kitongoji cha Chang'andu mapema mwaka huu,
wachomaji hawakuchukuliwa hatua.
Hali
hiyo ilimtokea Ngonyani mwishoni mwa wiki ambapo akiwa ameambatana na Mkuu wa
Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa, ambaye alifika Kijiji cha Magamba- Kwalukonge
kuzungumza na wananchi tangu mkasa huo utokee hivi karibuni, Gallawa alimtaka
Ngonyani kuzungumza na wananchi wake.
Ngonyani alisema
baadhi ya watu wamesema anawapendelea wakulima kuliko wafugaji na kufikia hatua
ya 'kuwashtaki' yeye na Mkuu wa Wilaya kwa Rais Kikwete, na kusema sio kweli
kwamba anawapendelea wakulima, bali wote ni wapiga kura wake na baada ya
kutokea kwa maafa hayo ya kuchomewa nyumba walifika mara kadhaa na Kamati ya
Ulinzi na Usalama ikiwa ni pamoja na kutoa vyakula kwa waathirika hao.
"Kuna watu
wamenichonganisha na Rais wangu kuwa napendelea wakulima kuliko wafugaji, hilo sio kweli,kwani kipindi chote cha matatizo yao..." alisema
Ngonyani. Hata hivyo alishindwa kuendelea na kwenda kukaa nyuma ya jukwaa huku
akibubujikwa na machozi.
Gambo alisema wote ni
wananchi wao, lakini suala la wafugaji kuingiza mifugo na kula mahindi karibu
ekari sita ni kuwaonea wakulima.
Alisema hata
waliochoma nyumba hawakuwa sahihi ndiyo maana waliamua kuwatuma wataalamu wa
ardhi na kwenda kupima matumizi bora ya ardhi kwenye Kijiji cha Magamba-
Kwalukonge na hali ya amani imerejea.
Mwananchi mmoja, Valentine Fwalo alimuelza Mkuu wa Mkoa mpango wa
matumizi ya ardhi huenda ukakwama baada ya baadhi ya wafugaji kukata kwa
mapanga vibao vinavyoonesha mipaka ya wakulima na wafugaji
No comments:
Post a Comment