Na Cresensia Kapinga, Songea
JESHI la Polisi mkoani
Ruvuma limemtia mbaroni, John Kasimila (56), mkazi wa Kijiji cha Ligera
kilichopo wilayani Namtumbo baada ya kukutwa akiwa na silaha mbili za moto,
risasi mbili na kilo 50 za nyama inayosadikiwa ni ya tembo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mchana ofisini kwake,
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Deusdedit Nsimeki, alisema kuwa tukio hilo
limetokea Julai 26, mwaka huu saa 9 usiku katika kijiji cha Ligela kwenye eneo
la mbuga ya wanyama ya Hifadhi ya Taifa ya Selous.
Inadaiwa siku hiyo ya tukio askari wa idara ya wanyama pori ambao
walikuwa kwenye doria kwenye mbunga ya Selous walifanikiwa kumkamata, Kasimila
akiwa na nyama inayosadikiwa kuwa ni ya tembo yenye uzito wa kilo 50 ambayo
ilikuwa imebebwa tayari kupelekwa Songea mjini.
Alisema kuwa Kasmila pia alikamatwa akiwa na silaha mbili za moto
ya kwanza ni aina ya Shotgun Grina yenye namba za usajili 461570 na silaha ya
pili ni aina ya liffle yenye namba 0019 ambayo ilikuwa na risasi mbili.
Silaha hiyo inasadikiwa ndiyo alikuwa ikitumika kuua tembo, ambapo
kwa hivi sasa kumekuwepo na matukio mengi ya kuuawa wanyama hao.
Alisema askari wa jeshi la polisi kwa kushirikiana na kikosi cha
kuzuia ujangili Kanda ya Kusini wanaendesha msako mkali wenye lengo la kutaka
kuwabaini wawindaji haramu waliokithiri kwenye mbuga ya wanyama ya Selous.
H a t a h i v y o K a m a d a Nsimeki, alisema kuwa Kasimil
ameshakamatwa na anaendela kuhojiwa na kwamba upelelezi wa tukio hilo
ukikamilika atafikishwa mahakamani
No comments:
Post a Comment