23 July 2013

MAUAJI JWTZ

  • KIKWETE ALIA NA UN
  • AITAKA IWARUHUSU WATUMIE SILAHA NZITO KUJIHAMI
  • ASISITIZA VIFO HIVYO HAVITAWAKATISHA TAMAA
    Picha ikionyesha tukio la kuagwa kwa askari saba wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Dar es Salaam jana, waliouwawa wakiwa katika operesheni za Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa (UNAMID),nchini Sudan hivi karibuni.

1 comment:

  1. Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi,
    Pia ningeomba serikali ya Tanzania ituambia mpango mzima wa usalama wa wanajeshi wetu huko Sudani,
    1. intelligence capability ya mazingira mana luck of intelligence ndo mana wameuwawa kama kumbikumbi

    2. Ubora wa silaha na zana za kivita walizo nazo, ni aina gani ya silaha wanapewa vijana wetu, kulinganisha na silaha za maadui ambao wanakua supported na kupewa silaha na nchi kubwa kwa ajili ya mafuta

    3. Training za kivita kulinganisha na natural geographical features, na serikali ituambie wanafanya mafunzo wapi achana na haya ya hapa tanzania ambayo ni duni ndo mana hata Rwanda wanataka watuchape.

    4.Future ya wanajeshi wetu waliobaki na serikali inasemaje usalama wao, wako chini ya nani, wangapi wako huko, na wanachukua order toka wapi, je ni utaratibu gani serikali inao ufanya wa kuwazungusha kati ya walioko huko na huku nyumbani

    5. Siongei kwa ghadhabu mana tumepoteza roho za raia wa tanzania wanao pigana nje ya nchi yao kwa kulinda maslahi ya nci nyingine, damu ya vijana imemwagika kwa kiapo ambacho hawajakiapa, kwamba NITAILINDA TANZANIA NA MIPAKA YAKE YOTE HADI TONE LANGU LA DAMU LA MWISHO.

    Mhariri naomba usinitie kapuni

    ReplyDelete