Revina John na Jazila
Mrutu.
UTAFITI umegundua
kuwa benki za kibiashara na taasisi binafsi katika nchi za Afrika Mashariki
huwa zinapoteza zaidi ya sh. bilioni 80 kwa mwaka kutokana na wizi wa
mitandaoni.Afrika
Mashariki kwa sasa inaundwa na nchi tano ambazo ni Tanzania,
Rwanda, Uganda, Kenya
na Burundi.
Hayo yalibainishwa jana jijini Dar es Salaam na Rais wa Taasisi huru ya kimataifa isiyokuwa ya Kiserikali inayohusika na Kusimamia na Kutoa Mafunzo na Maarifa ya Mifumo ya Mitandao hapa nchini (ISACA), Boniface Kanemba wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Kanemba
alisema kuwa, wizi wa mitandao umekuwa ukifanyika sana katika benki na taasisi mbalimbali
zisizokuwa za kiserikali ambapo kiasi hicho cha fedha huwa zinaibwa kila mwaka."Pia
matumizi ya huduma za kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu za mikononi
yameongezeka kwa kasi, hivyo kuongeza matukio ya wizi yanayohusiana na miamala
yake," alisema Rais huyo.
Aliongeza
kuwa, mbali na wizi wa fedha kampuni binafsi zikiwemo taasisi za kiserikali
zinapoteza taarifa nyingi zikiwemo zile binafsi na nyaraka muhimu za matumizi
ya ofisi bila kujua."Kutokana
na wizi wa mitandao wa muda, taasisi yetu imeandaa semina ambayo itahusisha
nchi tano za Afrika Mashariki, kampuni kutoka nchi za Ulaya, Amerika na Afrika
Kusini,ikiwa na lengo la kuelimisha juu ya matumizi ya kompyuta na mitandao
yake katika nyanja zote," alisema.
Alisema kuwa, semina hiyo itachukua siku tatu kuanzia Julai
28-30 mwaka huu mkoani Morogoro ambapo itafunguliwa na Naibu Waziri wa
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
No comments:
Post a Comment