02 July 2013

MAMA SALMA AHIMIZA MATUMIZI BIDHAA ZA NDANI


N a A n n a N k i n d a , (MAELEZO)

WA T A N Z A N I A wametakiwa kujifunza kuthamini vitu vya kwao na kuona kuwa ni bora zaidi kwa kufanya hivyo hata wageni watavipenda kwani bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi hazitapandishwa thamani na watu kutoka nje.
Mwito huo umetolewa juzi na mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kutembelea maonesho ya 37 ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika uwanja wa Mwalimu Nyerere uliopo Barabara ya Kilwa
wilayani Temeke jijini Dar es Salaam.

Mama Kikwete aliambatana na mke wa Mfalme Mswati wa Swaziland Inkhosikati Lambikiza, mke wa Makamu wa Rais wa Zambia, Mama Charlotte Scott na Mwakilishi wa mke wa Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Watu wa Congo ambaye ni Waziri wa Jinsia, Watoto na Familia Inagosi Bulo.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), alisema kuwa, walitembelea maonyesho hayo ili kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa ndani na nje ya nchi kuanzia ngazi ya juu hadi chini.
"Tumeona bidhaa za aina mbalimbali zinazozalishwa ndani na nje ya nchi na jinsi watu wanavyoweza kubadilishana uzoefu wa biashara hakika kadri siku zinavyozidi kwenda kuna maboresho makubwa juu ya utengenezaji wa bidhaa zinazozalishwa nchini," alisema Mama Kikwete.
Al iwa s h u k u r u wa g e n i alioambatana nao kwa kuzipenda bidhaa zilizopo kwenye mabanda ya Watanzania na kuwaomba wananchi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Dar es Salaam kutembelea maonyesho hayo kwani kuona ni kujifunza.
P i a a l iwa p o n g e z a n a kuwashukuru wanawake kwa kazi kubwa wanazozifanya za kuzalisha bidhaa na kufanya biashara mbalimbali ambazo zimewasaidia kujiletea maendeleo yao na jamii inayowazunguka.

No comments:

Post a Comment