SHIRIKA lisilo la kiserikali, Financial
Sector Deepening Trust (FSDT) limesema kuwa kampuni za simu nchini bado zina
nafasi kubwa kuhakikisha kuwa sekta ya kilimo inakua kupitia ubunifu wanaoweza
kuufanya, anaripoti Christina Mokimirya.
Mkurugenzi wa musuala ya ufundi, FSDT,
Bw. Sosthenes Kewe aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam
kuwa kupitia ubunifu, kampuni hizo za simu zinaweza kusaidia urahisi wa
upatikanaji taarifa mbalimbali kwa wakulima na wadau wengine wa kilimo.
Hi v i k a r i b u n i , k amp u n i
mbalimbali za simu za mikononi zilizindua huduma kupitia mitandao yake ambapo
wakulima watapata taarifa mbalimbali kuhusu shughuli za kilimo.
Kampuni ya simu za mkononi ya Zantel
kwa ushirikiano na Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika na kampuni ya
Sibesonke Limited zilizindua huduma za simu kupitia mtandao huo ambapo wakulima
wataweza kupata taarifa kwa urahisi na kwa wakati kuhusu njia bora na za kisasa
za kilimo kupitia huduma inayojulikana kama Z-KILIMO.
Kupitia huduma hiyo ya Z-KILIMO,
wakulima vijijini wataweza kupata taarifa sahihi na kwa wakati na hivyo
kuendeleza sekta hiyo nyeti kwa maendeleo ya nchi.
"Tunapongeza hatua kama
hizi, lakini bado juhudi zaidi zinatakiwa ili kufikia walengwa wengi zaidi”
alisema
No comments:
Post a Comment