12 July 2013

HALMASHAURI ZAONYWA KUACHA KUSUBIRI BAJETI YA SERIKALI


Na Florah Temba, Same
HALMASHAURI za wilaya mkoani Kilimanjaro zimetakiwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kutafuta vyanzo vingine vya mapato, vitakavyowasaidia kupata fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo badala ya kukaa kusubiri bajeti za Serikali.
Rai hiyo ilitolewa jana wilayani Same na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama wakati akikabidhi vifaa vya kupima ardhi katika halmashauri ya wilaya hiyo vyenye thamani ya sh. milioni 38 na gari kwa ajili ya ukusanyaji mapato lenye thamani ya Sh.mil.73.25 ambavyo vimenunuliwa na halmashauri hiyo kwa lengo la kupima kuongeza mapato ya Halmashauri.

Gama alisema ni lazima halmashauri za wilaya ziwe na ubunifu na zitafute vyanzo vingine vya mapato, ili kuondokana na utegemezi wa bajeti ya Serikali ambayo imekuwa haitoshelezi kufanya shughuli zote za kimaendeleo katika halmashauri.
"Bila kuwa na ubunifu wa kutafuta vyanzo vya mapato hamuwezi kuendesha halmashauri na badala yake mtaendelea kulalamika, sasa niwatake muache kufanya kazi kwa mazoea na mtafute vyanzo vingine vya mapato," alisema Gama.
Aidha Gama aliipongeza halmashauri hiyo kwa kutafuta njia ya kuongeza mapato katika halmashauri na kuwataka watendaji kuhakikisha vifaa vilivyonunuliwa vinatumika katika malengo yaliyokusudiwa.
Alisema wapo baadhi ya watumishi ambao wamekuwa wakikabidhiwa mali za umma na kuzifanyia ubadhirifu, hali ambayo Serikali haitaweza kuifumbia macho na badala yake itahakikisha wale wote watakaobainika kufanya hivyo wanawajibishwa na kuchukuliwa hatua.
Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Joseph Mkude kuangalia namna ya halmashauri hiyo itaweka utaratibu wa kuingia mkataba na wale watakaokabidhiwa vifaa ili kuwa rahisi kuwawajibisha pindi watakapovifanyia hujuma na ubadhirifu.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Same, Mkude alisema uwepo wa vifaa hivyo kutaiwezesha halmashauri hiyo kupima viwanja ambapo kwa sasa imelenga kupima viwanja 3, 000 lengo likiwa ni kuweka mji katika hali ya mpangilio.
Aliongeza kuwa halmashauri hiyo pia imenunua gari aina ya Toyota Hilux Double cabin kwa gharama ya shilingi milioni 73.25, fedha ambazo zimetokana na mapato ya ndani ya halmashauri hiyo na vyanzo vingine vya vilivyoko nje ya bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2012/13.
"Gari hili limelengwa kutumika katika idara ya fedha kitengo cha mapato, pamoja na kazi zingine ili kuweza kuboresha shighuli za ukusanyaji wa mapato katika halmashauri yetu, lakini pia ununuzi wa vifaa vya kupimia ardhi ni hatua kubwa katika kuhakikisha mji unapangwa na wananchi

No comments:

Post a Comment