Na Florah
Temba, Same
SERIKALI imekabidhi nyumba nane za
waathirika wa maporomoko ya ardhi yaliyotokea Novemba 2009 katika Kijiji cha
Goha Kata ya Mamba Miamba wilayani Same mkoani Kilimanjaro ikiwa ni utekelezaji
wa ahadi ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa wakati alipotembelea eneo hilo baada
ya kutokea kwa maporomoko.
Katika maporomoko hayo watu 24 walipoteza maisha huku kaya 8
zikikosa mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kuathirika na maporomoko hayo.
Akikabidhi nyumba hizo jana kwa niaba ya Rais Kikwete, Mkuu wa
Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama aliutaka uongozi wa wilaya kuhakikisha
nyumba hizo zinabaki kuwa mali ya watu hao kama ilivyokusudiwa na Serikali na
si vinginevyo.
Gama alitoa
agizo kwa uongozi wa wilaya kusimamia nyumba hizo ili wasiwepo watu wa kubadili
umiliki wa nyumba za wahanga hao na kwenda kwa umiliki wa watu wengine.
"Ninauagiza
uongozi wa wilaya kuhakikisha unasimamia nyumba hizi ili zibaki kuwa mali ya
wahanga na wasiwepo watu wa kuja kuwadanganya hawa watoto wadogo na kuwapatia
fedha kununua nyumba hizi na kubadili umiliki," alisema Gama.
Gama
aliongeza kusema kuwa ni vyema wilaya ikaweka utaratibu wa kuwepo kwa rekodi
halali ya umiliki wa nyumba hizo kisheria ikiwa ni pamoja na wahanga hao
kuhakikisha wanazitunza na kuzilinda ili ziweze kudumu.
Akitoa
taarifa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Joseph Mkude alisema
katika utekelezaji wa ujenzi wa nyumba hizo Ofisi ya Waziri Mkuu kitengo cha
maafa kilituma fedha shilingi milioni 162. 3 huku Benki ya NMB ikitoa mchango
wa saruji mifuko 100 na mabati 400 vyenye thamani ya shilingi milioni 9.7
No comments:
Post a Comment